Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi ya Waziri Mkuu kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Ally Mohamed Keissy

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkasi Kaskazini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi ya Waziri Mkuu kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. ALLY K. MOHAMED: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kunipa nafasi jioni ya leo.
Waheshimiwa ndugu zangu Wabunge, ukiona mtu kapigika ujue amekwisha. Ndugu zangu wameshaona, wameshafanya utafiti huko nje, hali zao ni mbaya, speed ya Magufuli inawatisha, walipania mwaka huu ndiyo waingie Ikulu, Ikulu ndiyo hawataiona tena kwa speed ya Magufuli. Sasa hawa jamaa ni wa kuonea huruma tu wameshapigika vibaya, hawajiwezi…
Mheshimiwa Magufuli anasifiwa dunia nzima. Kwa ushahidi Nigeria nimesikia Nigeria wanamsifu, Kenya wanamsifu, Uarabuni wanamsifu, Ulaya wanamsifu, hapa wanakaa wanampiga vijembe!
Mheshimiwa Mwenyekiti, hiyo Katiba amevunja Katiba gani? Katiba kuwasaidia mafisadi kutuibia pesa? Mimi nilizungumza hapa Bungeni, mafisadi wauwawe mapema na makaburi yao yawekwe minyororo, nilimwambia Mheshimiwa Magufuli…
Kwanza hawa jamaa hakuna haja ya Kuwapeleka Mahakamani. Haiwezekani mtu ana nyumba 70 bado unampeleka mahakamani, alipata wapi? Wewe tuchukue watu wa vijiweni, nenda pale Nyerere Square wako watu wanahangaika pale. Wako tayari kufungwa miaka miwili miwili wapewe milioni 100 wako tayari, itakuwa fisadi unamfunga miezi sita au unampa kifagio anafagia Sinza akitoka anakula mabilioni ya shilingi ya hela? Haiwezekani!
Mheshimiwa Mwenyekiti, hawa wameshaona wamepigika, speed ya Magafuli inawatisha, hawana chao, iliyobaki jiungeni na CCM mapema.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nilitaka kugusia habari ya mapato ya Serikali, mapato ya Serikali yanavyopotea katika nchi hii.MHE. ALLY K. Mheshimiwa Mwenyekiti, nilitaka kugusia habari ya mapato ya Serikali, mapato ya Serikali yanavyopotea katika nchi hii.
Ninyi tulieni mmeshakwisha, speed ya Magufuli inawatisha, hamna leo, hamna lolote, mnajiona mmefanya utafiti huko nje hamuungwi mkono na wananchi wote. Mlituambia hapa hapa Bungeni kwamba tukapimwe akili zetu kama tunamuunga Mheshimiwa Lowassa!
Je, ninyi mlipimwa akili zenu wakati mnamuunga Lowassa? Mlifanya utafiti, mliandika na vitabu, mkapita nchi nzima kumwambia Lowassa ni fisadi, je, mmepokeaje huyo fisadi mwenzenu? Sasa mmegeuka ninyi ndiyo mmekuwa mafisadi, CCM imekuwa safi, tulieni.
Magufuli speed anayokwenda nayo ni hiyo hiyo hamna kupunguza, hamna kupunguza aendelee zaidi ya mara mbili au mara tatu, hamna chenu. Tumepewa wajibu wa kuiongoza Serikali kwa miaka mitano na mmeona speed inavyokwenda mkajua mwaka 2020 hamtapata kura, hamkutegemea speed hiyo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nazungumzia vinasaba. EWURA waliingia mkataba vinasaba na shirika moja bila kupitia tenda, huyo jamaa anajichukulia kila mwezi shilingi bilioni 9.8, tulieni ninyi vimeshawauma hivi hampati kitu!
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu vinasaba anavyotumia EWURA kuweka kwenye Mafuta. Vinasaba vinagharimu shilingi 12.50. Vinasaba vyenyewe gharama yake ni shilingi 5.25 na mwenye vinasaba huyo mwenye hiyo kampuni anapata shilingi 7. Kwa hiyo anakusanya kila lita kwa mwezi jumla anapata shilingi bilioni 14 amekaa tu bila sababu yoyote!
Ndugu zangu wakati anaingia Mkataba Waziri Mkuu alikwa ni Mheshimiwa Lowassa ambaye mmemnadi nchi nzima, na hii kampuni ya vinasaba ni Lowassa ana ushirika ndani yake, vinasaba vya Lowassa. Ni kampuni ya Lowassa na ndiyo alituingiza mkenge, ni Lowassa alipokuwa Waziri Mkuu.
Hili fisadi, anachukua Lowassa kila mwezi shilingi bilioni 14 hii kampuni yake, sasa ndiyo nawaambia mkakae mkachunguze huko. Mafisadi wakubwa. Mnaniharibia hata kuchangia kwangu. Mmemnadi ninyi nchi nzima, juzi ndugu yangu Mheshimiwa Khatib hapa anasema mwaka 2020 mtamleta yule yule Mheshimiwa Lowassa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana Serikali ilipiga marufuku kuagiza sukari nje. Ninachowaomba, wapige marufuku kuagiza mchele kutoka nje. Kuna mchele kutoka India, kutoka Thailand katika nchi yetu hii wakati mchele wetu uko mwingi, tuokoe hela za kigeni kama tunavyofanya mambo ya sukari.
Mheshimiwa Mwenyekiti, haiwezekani kuagiza mchele nchi za nje wakati tuna mchele umerundikana Kyela, Tunduma, Sumbawanga. Kwa hiyo upigwe marufuku mchele kuingizwa kama ilivyopigwa marufuku sukari ili kuokoa wakulima wetu.
Kuhusu usafiri mwambao wa Ziwa Tanganyika, Serikali ya Awamu ya Nne ilituahidi meli mbili, ninashangaa hata Awamu ya Tano hata meli hakuna ni kukarabati MV Liemba tu! Sasa inakuwa ni matatizo, hakuna cha kutengeneza meli mbili, hata hiyo moja nimeona kuna ukarabati MV Liemba. MV Liemba ina umri wa miaka 112, hatukatai kukarabati MV Liemba, ikarabatiwe, lakini tunahitaji na meli mpya.
Kuhusu suala la uvuvi, wavuvi wetu katika Ziwa Tanganyika wako duni sana. Tunaomba wafikiriwe ili na wao waweze. Zambia ina asilimia sita ya maji ya Ziwa Tanganyika lakini Zambia ndiyo inakuwa muuzaji mkubwa wa samaki na dagaa, ina asilimia sita ya maji lakini ndiyo muuzaji mkubwa wa dagaa na samaki za Ziwa Tanganyika, wakati sisi tuna asilimia 38 ya Ziwa Tanganyika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu Idara ya maji, nimezungumza sana habari ya idara ya maji ni majipu na Namanyere. Siyo lazima kumngoja Rais au Waziri Mkuu nimezungumza mara kwa mara hapa. Wanaiba, wameandika gari hewa Dar es salaam na Namanyere na mabomba hewa hakuna kilichopelekwa, kila mara nazungumza hapa, ni hewa tupu hakuna kitu kinachofanyika!
Mheshimiwa Mwenyekiti, Namanyere wananchi wana taabu ya maji miaka na miaka, wananidanganya hapa eti watanipa bilioni tatu, hamna cha bilioni moja, wala 500 milioni. Kwa hiyo, naomba bajeti ya safari hii, mradi wa maji na Namanyere ipewe kipaumbele.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu suala la mafisadi hukumu yao haitoshi kuwapeleka tu mahakamani. Haiwezekani mtu anakamatwa na nyumba 70 au 40, Serikali inachukua muda kumpeleka mahakamani na anapata dhamana.
Kwanza naiomba Serikali zile nyumba zinyang’anywe, kama alikuwa polisi, nyumba ziende Polisi, kama alikuwa mtu wa TRA (Tanzania Revenue Authority) ili wafanyakazi wa TRA wakodishe zile nyumba. Haiwezekani wewe mtu umefanya kazi yako inajulikana mshahara wako ni mdogo leo unanunua nyumba 40 au 70.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu mapato na matumizi ya Bunge, Wabunge wengi nilizungumza hata mara ya kwanza hapa, wanasafiri kama wakimbizi wa Burundi. Wanapishana airport kama Wakimbizi, Magufuli amedhibiti hii wanaanza kumpiga vita, ndugu zangu kwa vipi? Mpaka timu za mpira zinakwenda kwa ndege Rwanda, hamna lolote!
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba apige marufuku timu zote za Bunge kwenda nje ya nchi. Safari za hovyo hovyo marufuku, Wabunge tuishi hapa tufanye kazi majimboni kwetu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, safari za nini kwenda nje? Hakuna cha kutoa safari kwa Wabunge, Wabunge tukae hapa hapa tufanye kazi kwenye Majimbo kwa wananchi waliotuchagua. Kwenda nje iwe marufuku na mimi ninamuunga mkono Mheshimiwa Magufuli azuie safari zote za Wabunge za michezo hovyo hovyo kwenda nje, Wabunge wakakae majimboni kwao baada ya Bunge kutekeleza majukumu yao Majimboni. Ahsante sana.