Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Mendard Lutengano Kigola

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kusini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. MENDRAD L. KIGOLA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naipongeza Serikali kwa mipango mizuri ya kuimarisha miundombinu ya barabara zinazounganisha mikoa na mikoa, wilaya na wilaya kwa kujenga kwa kiwango cha lami. Pia naipongeza Serikali kwa kujenga barabara ya kutoka Dodoma – Iringa na Iringa - Mafinga.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naiomba Serikali kumalizia kujenga barabara ya Mafinga hadi Chimara; Barabara ya Nyololo hadi Igowole - Kibao – Mtwango (kilomita 40); barabara ya Mafinga hadi Mgololo (kilomita 84) na barabara ya Igowole – Kasanga -Nyigo. Barabara hizi ni ahadi ya Rais pia mipango ya Chama cha Mapinduzi (CCM), ukurasa wa 71 imeandikwa. Barabara ya Nyololo –Igowele - Mtwango (kilomita 40), upembuzi yakinifu ulishafanyika mwaka 2013/ 2014 na 2014/2015 Serikali iliahidi kujenga barabara hiyo kwa kiwango cha Lami.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.