Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Hamida Mohamedi Abdallah

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Lindi Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. HAMIDA M. ABDALLAH: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kumpongeza Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano na timu yake kwa utekelezaji wa miradi mbalimbali kwa kipindi hiki cha 2016/2017 lakini kwa maandalizi ya utekelezaji wa mpango huu wa 2017/2018.

Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kwa dhati kuishukuru Serikali kwa kufanya usanifu kilomita 91 za barabara za Masasi – Nachingwea - Nanganga kwa kiwango cha lami. Hata hivyo, kwa barabara za mkoa ambazo zipo katika mpango wa mwaka 2017/2018 kilomita 537.9, naiomba Serikali kuiangalia barabara itokayo Nachingwea – Liwale kwani hali si shwari, kipindi cha masika barabara hiyo haipitiki kabisa. Naiomba Serikali kuingiza katika mpango wa bajeti ijayo ya mwaka 2018/2019.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Uwanja wa Ndege wa Lindi ni mkongwe sana na ulitumika hata kipindi cha Ukoloni na ni kiwanja bora katika Afrika ulikuwa namba tatu. Kwa hiyo, naomba sana Serikali kuhakikisha uwanja wa Lindi unapewa kipaumbele ukizingatia Lindi sasa tunategemea uwekezaji mkubwa wa kiwanda cha LNG.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niipongeze Serikali imeweza kutuunganisha Watanzania kupitia sekta ya mawasiliano.

Bado katika Mkoa wa Lindi tuna vijiji havina kabisa mawasiliano. Kwa mfano, Nachingwea (Kijiji na Mbondo); Ruangwa (Nangurugai na Nandandala); Kilwa (Mandete, Mandawa, Mavuji na Kandawale) na Liwale (Ngongowele, Mirui, Mlembwe na Mpigamiti). Naomba Serikali kupitia Mfuko wa UCSAF kuvisaidia vijiji hivi viweze kupata mawasilino.

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema haya, naunga mkono hoja kwa asilimia mia moja. Ahsante sana.