Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Martha Jachi Umbulla

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. MARTHA J. UMBULLA: Mheshimiwa Mwenyekiti, namshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunijalia uzima na afya na kuweza kuchangia hoja hii. Mchango wangu ni kama ifuatavyo:

(i) Fedha zinazotengwa na kuidhinishwa na Bunge kwa ajili ya ujenzi wa barabara zinachukua muda mrefu sana kutolewa na Hazina na pengine itolewe kidogo sana na hivyo kutokidhi ukamilishaji wa barabara zetu. Hali hii imeathiri sana ujenzi wa barabara zinazounganisha Mkoa wetu wa Manyara Makao Makuu Babati na Wilaya zake zote kwa kiwango cha lami. Matokeo yake hali hii ya kutokuwa na barabara za uhakika, hasa wakati wa masika, inarudisha nyuma uchumi wa mkoa na wilaya zote za mkoa wetu ambazo ziko pembezoni, bila barabara hali ya wananchi inabaki kuwa duni sana, hususani Wilaya za Mbulu, Simanjiro, Kiteto na Babati Vijijini. Tunaomba Serikali itoe fedha kwa wakati kwa barabara zote zilizo ndani ya Ilani ya CCM 2015- 2020 mfano barabara ya Kondoa – Kibaya – Kongowa; barabara za Babati – Dareda – Haydom - Mbulu na barabara zote zilizoko kwenye njia kuu za kiuchumi.

(ii) Serikali ibuni utaratibu mzuri wa kuboresha manunuzi ya umma. Uzembe na kukosa uaminifu kunasababisha kujenga miundombinu hafifu ya barabara na sekta nyinginezo zilizo ndani ya Wizara ya Ujenzi.

(iii) Serikali pia iweke fedha ya kuboresha Uwanja wa Ndege wa Arusha ambao sasa hivi hauruhusu ndege kubwa kutua. Uwanja huo utasaidia sana kwa sababu sasa hivi wageni wengi, wakiwepo watalii wengi wanatua KIA wanaelekea Arusha. Hivyo wakitua Arusha moja kwa moja itawawia rahisi kufika Arusha saa 1.30 bila adha ya kuandaa shultle na kuchukua muda mrefu kuliko muda waliotumia toka Dar es Salaam KIA kwa ndege (dakika 45-50).

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha.