Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Stephen Hillary Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Korogwe Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. STEPHEN J. NGONYANI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kumekuwepo na tabia ya kusahau barabara ya Korogwe – Dindira – Bumbuli - Somi kwa kiwango cha lami tangu mwaka 2010 hadi leo wakati barabara hii imo ndani ya Ilani Uchaguzi ya Cham cha Mapinduzi ya mwaka 2010. Kila siku inasahaulika na cha kusikitisha mwaka huu wa fedha 2017/ 2018 imetengewa kiwango kidogo cha fedha cha sh. 130,000,000/=, hii haina msaada wowote. Pili, Mji Mdogo wa Mombo uliahidiwa kuweka kiwango cha lami tangu mwaka 2014 hadi leo hakuna msaada wowote ambao umefanyika, kila kukicha maneno tu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara za mkoa hadi leo zinajengwa chini ya kiwango kiasi ambacho fedha zinatengwa lakini utengenezaji wake si wa kuridhisha. Fedha zinahamishwa bila sababu yoyote, kwa mfano barabara ya Korogwe – Magoma – Maramba – Mabokwemi kuna sehemu hazikumaliziwa kabisa. Barabara ya Korogwe – Mnyuzi – Maguzoni kuna kama kilometa 15 zilitakiwa heavy grading lakini hata kilometa tisa hazikufanyika. Sasa Serikali iliangalie suala hili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna barabara zinatakiwa kupandishwa hadhi kutoka za Wilaya kuwa za Mkoa. Hadi leo hakifanyiki chochote wakati DCC imepitisha RCC imepitisha. Barabara hizo ni hizi zifuatazo:-
(a) Barabara ya kutoka Mombo hadi Mzeli inaunganisha wilaya mbili na Mkoa kwa ujumla;
(b) Barabara kutoka Makuyuni hadi Mpakani Bumbuli; na
(c) Barabara ya kutoka Msambiazi hadi Bungu na kuunganisha Wilaya Bumbuli haijafanyiwa chochote.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mawasiliano. Kuna Kata ya Kizara mawasiliano hakuna, kuna Kata ya Kalalami katika Kijiji cha Kigwasi (wachimbaji wa madini) na inapakana na Mbuga ya Wanyama ya Mkomazi hakuna mawasiliano. Serikali isiangalie tu mjini na huku wapo wananchi wenu. Nategemea Mheshimiwa Waziri atakuja na majibu mazuri.