Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Joseph Michael Mkundi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukerewe

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. JOSEPH M. MKUNDI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuchangia yafuatayo:-
Kwanza, Usafiri wa Majini. Vivuko; Kivuko, cha MV Nyerere kinachofanya kazi kati ya Bugorola – Ukara, kina matatizo makubwa ya kuchoka/ubovu wa engine zake zote mbili, hali iliyopelekea mara kwa mara kuzua taharuki kwa wasafiri kutokana na kuzima ikiwa katikati ya maji. Jambo hili ni hatari sana kwa maisha ya abiria na hata kinapofanya safari zake kivuko hiki kinatumia karibu masaa mawili kwa umbali huo badala ya nusu saa hadi dakika 45.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ushauri; zinunuliwe engine nyingine kwa ajili ya kivuko cha MV Nyerere ili kuepusha matatizo yanayoweza kuhatarisha maisha, pia Serikali ione umuhimu wa kutengeneza kivuko kwa ajili ya wakazi zaidi ya 20,000 wa Kisiwa cha Irungwa na Nansio ambao wanatumia mitumbwi na hivyo kusafiri kwa zadi ya masaa matano (5) wakiwa majini. Awali MV Ukara ilikuwa inafanya kazi eneo hili kabla ya kuharibika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu meli; kuharibika kwa meli ya MV Butiama na uchakavu wa meli ya MV Clarius kumepunguza ufanisi na kuleta shida ya usafiri kati ya Mwanza – Nansio. Ushauri wangu ni kwamba, mchakato wa matengenezo ya meli ya MV Butiama ukamilike haraka ili meli hii iweze kutoa huduma na kupunguza tatizo lililopo la usafiri. MSCL ipewe fedha za kutosha ili iweze kuboresha meli ya MV Clarius ili meli hiyo iweze kumudu ushindani na kushindanishwa kibiashara.

Pili, Mawasiliano; kuna tatizo kubwa la mawasiliano kwenye baadhi ya maeneo yakiwemo eneo la Bwasa na Bukiko, wananchi katika maeneo haya hupanda vilimani ili kupata mawasiliano. Ombi langu, ijengwe minara kwa ajili ya mawasiliano; Bukiko katika Kata ya Bukiko na Bwasa katika kata ya Igalla.

Tatu, Barabara; barabara ya Bunda – Kisorya – Nansio ambayo ni muhimu sana kwa uchumi wa maeneo haya inajengwa kwa kasi ndogo sana. Barabara hii ikamilike mapema ili iweze kutoa huduma kwa wananchi wa maeneo haya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali iweke katika bajeti ya kila mwaka mpango wa kujenga kilomita moja kila mwaka kwenye barabara ya Bulamba – Mavutunguru – Kakukuru badala ya kutumia fedha nyingi kila mwaka kwa ajili ya kufanya ukarabati usio na tija katika barabara hiyo. Fedha hiyo iongeze kilomita moja (1) ya lami kila mwaka kwenye hiyo barabara.

Mheshimiwa Mwenyekiti, formula ya ugawaji wa fedha za Mfuko wa Barabara ibadilishwe na kutoa mgao ulio sawa kati ya TANROADS na Halmashauri za Wilaya. Hii itawezesha Halmashauri kuwa na uwezo wa kutengeneza barabara nyingi zinazosimamiwa na Halmashauri zetu ambazo zinakabiliwa na uharibifu mkubwa lakini hazina uwezo wa kuzihudumia kikamilifu.