Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Anthony Calist Komu

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Moshi Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. ANTONY C. KOMU: Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote nimshukuru Mheshimiwa Waziri na wasaidizi wake kwa jitihada walizofanya na hasa kutukumbuka sisi watu wa Moshi Vijijini. Katika Hotuba ya Mheshimiwa Waziri katika Sub-vote 2005 - Roads development divisions kasma 4115 (vii) inaonesha tumetengewa sh. 811,000/= Kiboroloni – Kiharara – Tsuduni – Kidia kilomita 10.8.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwaka wa fedha unaoishia wa 2016/2017, tulitengewa shilingi bilioni 2.583; lakini mpaka leo hakuna hata shilingi moja iliyotolewa kwa barabara hii ambayo ni muhimu sana. Ukiacha shughuli nyingine za kiuchumi zilizopo katika maeneo inapopita barabara hii ambazo nyingi ni za kitalii, barabara hii ndiyo iendayo kwa wakwe wa Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu Mheshimiwa Benjamin William Mkapa, nyumbani kwa Mama Anna Mkapa. Ni imani yangu kuwa inafaa sana kuwaenzi wazee wetu hawa kwa kuwapa barabara nzuri. Naomba sana bajeti ya mwaka jana isipotee, zifanyike jitihada za makusudi ili kazi hii iweze kuanza kupitia fedha za mwaka unaoishia wa 2016/ 2017.

Mheshimiwa Mwenyekiti, chini ya miradi ya barabara za mikoa (kasma 4132) 2017/2018, Mkoa wa Kilimnjaro kuna ukarabati wa Kibosho Shine – Mto Sere Road). Upgrading to Dar es Salaam of Kibosho Shine – kwa Raphael International School Road, kilomita 27.5 zimetengwa shilingi milioni 128.00.

Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara hii ilikuwa ni ahadi ya Rais wa Awamu ya Nne Mheshimiwa Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete na ilianza kujengwa kwa kiwango cha lami takribani kilometa saba. Naomba sana Mheshimiwa Waziri aangalie uwezekano wa kukamilisha ahadi hii kwa ukamilifu wake kwa kiwango cha lami. Aidha, tumetengewa Rehab, Uru – Kishumudu Parish – Materuni Road, kilometa nane shilingi milioni 61.00. Barabara hii ilijengwa kwa kiwango cha lami miaka ya 1970 mwanzoni, imebomoka karibu yote. Mwaka wa jana 2016 ilijengwa sehemu ndogo kwa kuondoa lami ya zamani na kuweka mpya urefu wa takribani kilometa 1.5.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kiasi hiki cha shilingi milioni 61.1 ni kidogo mno kuendeleza kazi hii ambayo imeliliwa mno na wananchi wa maeneo hayo. Barabara hii ni njia ya utalii kwenda Mlima Kilimanjaro Maanguko ya Mnambeni na katika mashamba ya kahawa. Namwomba sana Mheshimiwa Waziri aliangalie upya suala hili la barabara hii, si vema kurudi nyuma, yaani kutoka lami kwenda changarawe. Tuko tayari kusubiri kwa kujengewa kidogo kidogo lakini lami.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho ni kuhusu kujengwa kwa kiwango cha lami barabara ya Mamboleo – Shimbwe ambapo ni ahadi ya Rais wa Awamu ya Tano, Dkt. John Joseph Pombe Magufuli. Namwomba sana Mheshimiwa Waziri, mikakati ya kuanza kutekeleza ahadi hii ianze.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ushauri wa kiujumla. Ingekuwa ni vema sana kama Wizara ingefanya survey ambayo ingeiwezesha Wizara kutambua mahitaji halisi ya kila barabara kwa maana ya kazi/mahitaji mahususi eneo kwa eneo. Mara nyingi nimeona kazi zikifanyika kwa mazoea tu wakati ingewezakana labda barabara A katika eneo fulani ikajengwa kwa kiwango cha lami hata kwa robo kilometa ikasaidia sana barabara hiyo kudumu kuliko kuiwekea changarawe na kushindilia na mvua moja tu ikaibomoa yote au ikaacha kupitika kabisa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha.