Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Halima James Mdee

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. HALIMA J. MDEE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ukurasa wa 22 wa hotuba ya Mheshimiwa Waziri inazungumzia upanuzi wa barabara ya New Bagamoyo (Morocco JCT) – Mwenge – Tegeta (12.9 kilomita). Barabara hii ilishakamilika na kuzinduliwa katika kipindi cha mwaka 2010/2015. Kwa maelezo ya Mheshimiwa Waziri barabara hii iko katika kupindi cha uangalizi kinachotarajia kukamilika 30 Julai, 2017. Ni ushauri wangu kwa Mheshimiwa Waziri na timu yake, wapite na kufanya uhakiki katika barabara husika kutokana na ukweli kwamba kuna maeneo ambayo tayari yameshaharibika (hayako katika hali nzuri).

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna maeneo ambayo wakati wa ujenzi wa barabara mapokea na matoleo ya maji hayakujengwa katika kiwango ambacho kinakidhi. Kiwango cha maji wakati wa mvua kinachotoka maeneo ya Goba ni kikubwa na hatari zaidi iko Tangi Bovu maeneo ya Mbuyuni, Kunduchi, Africana pamoja na Salasala. Kutokana na ufinyu huu kuna hatari ya barabara kupasuka na kuharibika. Ni ushauri wangu kwa Mheshimiwa Waziri na kwa Wizara kuchukua hatua za dharura ili kunusuru kazi iliyokwishafanyika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, natambua kwamba kuna kazi inayoendelea ya Ujenzi wa service road katika barabara husika. Kwa muktadha huo huo, ningependa kujua kwamba ni lini taa za barabarani zitakamilika kwa kuwa ajali nyingi zinasababishwa na kutokuwepo kwa taa barabarani?

Mheshimiwa Mwenyekiti, hotuba ya Mheshimiwa Waziri katika ukurasa wa 22 na 23 inaonesha kwamba kipande cha Morocco – Mwenge kitajengwa kwa kiwango cha dual carriage way. Baada ya kupata msaada wa fedha kutoka Serikali ya Japan kupitia Shirika la Ushirikiano wa Kimataifa la Japan (JICA). Hata hivyo, hotuba za bajeti za miaka minne iliyopitia ilionesha kwamba Serikali ya Japan ilitoa bilioni 88 ambapo pamoja na mambo mengine ingejenga barabara ya Mwenge – Tegeta (first phase) na Mwenge – Morocco (second phase)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kupata ufafanuzi juu ya utata uliojitokeza kutokana na kauli mbiu zinazotofautiana kutoka kwa Serikali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, imekuwa ni utamaduni kwa Mfuko wa Barabara kutoa kiasi fulani cha fedha kwenda halmashauri, lengo likiwa ni kuziwezesha halmashauri zetu ambazo zina uwezo mdogo. Hata hivyo, kwa mwaka wa fedha 2016/2017, Manispaa ya Kinondoni ilitarajia kupata Shilingi bilioni 10.5 kutoka Mfuko wa Barabara. Mpaka kikao chetu cha mwisho cha Baraza la Madiwani taarifa tulizopewa ni kwamba hakuna hata shilingi iliyowasilishwa Halmashauri, hali ambayo imeathiri kwa kiwango kikubwa utekelezaji wa miradi ya maendeleo. Naomba ufafanuzi ni lini fedha husika zitaletwa?

Mheshimiwa Mwenyekiti, TAZARA. Kwa muda wa miaka miwili/mitatu mfululizo nimekuwa nikizungumza juu ya uuzwaji wa nyumba za TAZARA kinyume na utaratibu halikadhalika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, uvamizi wa maeneo ya TAZARA yaliyofanywa pasipo hatua zozote kuchukuliwa. Mheshimiwa Samwel Sitta (marehemu) akiwa Waziri mwenye dhamana ya Wizara ya Uchukuzi nilimpatia Audit Report ikizungumzia kwa kina suala tajwa hapo juu lakini hakuna hatua yoyote iliyochukuliwa mpaka sasa kuhusiana na suala husika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, natambua hatua zilizoanza za ujenzi wa barabara za Tegeta kibaoni – Wazo Hill – Goba. Taarifa zinaonesha kwamba kumpata mkandarasi kwa ajili ya sehemu ya Maendeleo – Goba (kilometa tano) zinaendelea. Ni imani yangu ahadi hii ya muda mrefu, itaanza kufanyiwa utekelezaji katika hatua ya kwanza kuelekea kukamilisha ujenzi mpaka Kibaoni.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kupata ufafanuni wa barabara kuu kuelekea Ruaha National Park itajengwa?