Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Eng. Gerson Hosea Lwenge

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. ENG. GERSON H. LWENGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze kumpongeza Mheshimiwa Waziri, Naibu Waziri na wafanyakazi wote wa Wizara hii kwa kazi wanayoifanya na kuliletea Taifa letu sifa kubwa. Hotuba ni nzuri na naunga mkono hoja hii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wilaya ya Wanging’ombe ina changamoto kwenye eneo la barabara kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza barabara ya Njombe – Mironga – Makete (kilomita 109). Hii ni ahadi ya Ilani ya Chama Tawala. Mheshimiwa Rais aliwaahidi wapiga kura wangu kwamba wakimpa kura na akaingia Ikulu itakuwa ni barabara ya kwanza kuanza kuijenga. Ni zaidi ya mwaka mmoja na nusu sasa yuko Ikulu na barabara hii haijaanza kujengwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara ya Njombe (Ramadhani) – Iyayi (kilomita 74). Barabara hii ni ya muhimu kwa uchumi wa Mkoa wa Njombe na hususan Wilaya ya Wanging’ombe. Barabara hii ilifanyiwa usanifu tangu Mwaka 2014 lakini sijaona kwenye Randama ya 2017/2018 kutengewa fedha za kujenga. Ni lini barabara hii itatengewa fedha za kujenga?

Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara ya Halali – Ilembula – Igwachanya - Itulahumba (kilometa 35). Barabara hii ni ya wilaya na nimemwomba Mheshimiwa Waziri kwamba ipandishwe daraja au ihamishiwe kwa Wakala wa Barabara (TANROADS). Barabara hii ni kiungo cha hospitali ya Ilembula (DDH) na Makao Makuu ya Wilaya (Igwachanya). Barabara hii ilifunguliwa na TANROADS kwa kutumia fedha za Mfuko wa Barabara tangu mwaka 2013 kwa maombi maalum. Sasa barabara hii kwa takriban miaka minne haijapata routine maintenance. Naomba sana Mheshimiwa Waziri ombi langu lifikiriwe kwani sijaona kwenye Randama kutengewa fedha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia naomba Wizara hii eneo la Makao Makuu ya Wilaya ya Wanging’ombe hayana mawasiliano ya uhakika ya simu. Mnara wa Vodacom umewekwa lakini hauna nguvu kabisa.