Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Yussuf Haji Khamis

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Nungwi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. YUSSUF HAJI KHAMIS: Mheshimiwa Mwenyekiti, nachukua fursa hii adhimu na muhimu kumshukuru Allah Subhanahu Wataala, kwa neema kubwa ya uhai na uzima. Pia nikushukuru kwa kuniruhusu nichangie mada iliyopo mbele yetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, maneno haya niliyazungumza katika hotuba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu lakini kwa umuhimu wa jambo lenyewe na Mheshimiwa Waziri ndiye mhusika mkubwa, naomba nirejee ili nipate jawabu muafaka. Mimi binafsi nimekufuata Mheshimiwa Waziri zadi ya mara tatu kukuelezea malalamiko ya wasafirishaji wa majahazi katika Bandari ya Dar es Salaam. Kwa bahati mbaya sana hukuwahi kukutana na wadau wa majahazi hata mara moja, jambo ambalo sikulaumu sana kwa sababu mchakato wa hapa kazi ni mkubwa sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, watu wa majahazi wanalalamika kipimo cha (CDM) ambacho CDM moja (1) wanalipa 7,500/=, ambapo (fuso) gari moja linajaa kwa CDM 80. Kwa fuso moja CDM 80 wanalipa sh. 600,000 ambapo mzigo huu walilipia Sh. 600,000/= wao wanabeba kwa thamani ya milioni moja 1,000,000/=. Kwa maana hiyo kama jahazi lina uwezo wa kubeba CDM 160 ama mafuso mawili Serikali inachukua 1,200,000/= na wenye jahazi wanabakiwa na laki 800,000/=, kwa hiyo wanalalamika hawapati kitu na biashara hii inawashinda.

Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda Mheshimiwa Waziri akutane nao wenyewe ili ajue kiini cha tatizo hili. Hata hivyo, naomba aiangalie suala hili na atoe tamko kuhusu malalamiko yao haya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa naomba nizungumzie usafiri wa bahari kati ya Tanga – Pemba – Nungwi. Usafiri wa sehemu hizi wa bahari umekuwa na matatizo makubwa na husababisha ajali nyingi kwa kutumia vyombo duni na hafifu sana. Wananchi wamelalamikia Serikali yao kuhusu kuwapatia usafiri wa hakika mwishowe mfanyabiashara mkubwa Said Bakhresa ameleta meli kubwa ambayo itatoa huduma katika maeneo hayo. Nichukue fursa hii kupongeza Kampuni ya Bakhresa kwa ufumbuzi wa tatizo hili. Angalizo, Bakhresa ni mfanyabiashara. Kwa hiyo, anahitaji faida katika biashara yake. Abiria wa Tanga na Pemba kuna wakati wanakuwa wengi na wakati mwingine wanapungua. Wasiwasi wangu kama upungufu wa abiria na mizigo utakuwa mkubwa unaweza kukatisha usafirishaji na wananchi kukosa usafiri wa hakika. Je, Serikali ina mpango gani kwa wananchi hawa kama hali itakuwa kama hivyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba Mheshimiwa Waziri akisimama anitoe wasiwasi wangu huu.