Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Mariamu Nassoro Kisangi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. MARIAM N. KISANGI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakamilisha mchango wangu wa maneno kuhusu barabara. Mabasi yaendayo kasi yaendelee kwa haraka kwenda Mbagala.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Bandari; ajira ndogo ndogo. Kuwe na mpango madhubuti wa kuzitambua ajira hizo na vijana wa Dar es Salaam hususani Temeke wapate ajira hizo, vile vile mwisho wa siku tupate takwimu za ajira hizo. Fungu la Bandari la Corporate Social Responsibility litolewe kwenye makundi mbalimbali ya wasiojiweza na wazee. Pia akinamama wajasiriamali wadogo watoto wa Kurasini, mama lishe na wauza vinywaji. Bandari iwajengee uwezo na kuwawekea mazingira mazuri ya kuuzia bidhaa zao. Vile vile hata Canteen ya Bandari iwajengee uwezo akinamama walete bidhaa kama vitafunwa ili nao wafaidike na bandari yetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Uwanja wa ndege. Ni vyema Serikali ikaelekeza mpango wa mabasi ya mwendo kasi kwenye uwanja huo. Hata hivyo sijaona eneo la biashara kuonesha bidhaa za Tanzania na utalii, je Serikali imepanga vipi eneo hilo?

Mheshimiwa Mwenyekiti, Reli; maeneo ya Shirika la Reli yaliyo mengi yametekelezwa kiasi cha kuwa Mafichio ya wezi na vibaka. Maeneo yatunzwe vizuri ili yatumike baadaye.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mawasiliano; matumizi makubwa ya simu yanafanyika Dar es Salaam, lakini ukitoa kodi tunayokata kama wana Dar es Salaam wanatusaidia nini moja kwa moja kama wananchi wa Dara es Salaam? Naomba Makampuni ya simu wakae na sisi Wabunge kuangalia namna bora ya kutuchangia watu wa Mkoa wa Dar es Salaam katika mipango ya maendeleo ya Mkoa wetu. Kikubwa na kuongezeka kwa gharama za simu kumekuwa na matangazo ya uongo kuwa kuna nafuu ya matumizi, ukiangalia dakika hakuna kitu badala yake weekend kuna ongezeko kubwa la gharama za simu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja kwa asilimia mia moja.