Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Charles John Mwijage

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muleba Kaskazini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. CHARLES J. MWIJAGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, kupitia njia ya maandishi naomba kuchangia Bajeti ya Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Barabara ya Muhutwe – Kamachumu – Muleba (kilomita 53). Barabara tajwa imeainishwa katika Ilani ya CCM ya mwaka 2015 kuwa itajengwa kwa kiwango cha lami. Umuhimu wa barabara hii kwa vipindi tofauti nimeelezea hapa Bungeni. Pamoja na mpango huu kwa sasa barabara hii imeharibika sana maeneo ya Rukono (Muhutwe – Kyabakoba) na Malele (Kyabakoba – Nyawaibewa). Uharibifu ni mkubwa sana kiasi kwamba kuna wakati watu watokao Muhutwe kwenda Kamachumu (15km) wamelazimika kuzunguka kupitia Muleba, umbali wa kilomita zaidi 110.

Mheshimiwa Mwenyekiti, maombi yangu ni kuwa mradi huu utekelezwe kama ilivyoanishwa katika Ilani yetu. Aidha, kutokana na hali ya barabara kutoruhusu usafiri kuwa salama naomba bajeti ya barabara tajwa kama inavyoonekana ukurasa 286 sehemu kubwa ihamishiwe chini
ya mpango wa upgrading to DSD. Nyongeza za fedha itasaidia kujenga maeneo korofi kwa zaidi ya kilometa sita zilizopangwa sasa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kupitia Bunge lako nieleze kutokuridhika na utendaji usioridhisha katika barabara hiyo kwa mwaka huu (2016/2017) hali iliyopelekea maeneo niliyoyaeleza hapo awali kuharibika. Muhimu watendaji wajiulize ni kwa nini kwa kipindi cha zaidi ya miaka 10 eneo hilo halijapata tatizo kama la sasa katika maeneo ya Rukomo, Ruhanda na Malele. Kutokana na hali ya udongo wa eneo husika mkandarasi atafanya kazi hewa, ufanisi hewa. Kuongeza na kushindilia tabaka la changarawe badala ya kupalula tabaka la changarawe ambalo limewekwa kabla. Siridhiki na utendaji wa eneo hilo na limekuwa chini ya mategemeo ya wananchi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mamlaka Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADs). Yamekuwepo mawazo ya kuanzisha mamlaka ya kusimamia barabara zilizoko chini ya Halmashauri. Hii ni kutokana na utendaji mzuri na wenye ufanisi wa TANROADs.

Mheshimi Mwenyekiti, utendaji na ufanisi wa TANROADs umefikiwa baada ya kujifunza na uzoefu wa muda mrefu. Hivyo badala ya kuanzisha Mamlaka Nyingine, basi baadhi ya barabara za halmashauri zipandishwe kwenda TANROADs na mgawo wa fedha za Bajeti uongezeke sawia. Halmashauri wabaki na eneo dogo la mtandao wa barabara; na kama nilivyoelekeza awali kwamba mgawo wao kutoka Road Fund upungue. Hata kwa mgao huu kwa halmashauri bado ufanisi wa barabara si wa viwango na si mzuri kutokana na upungufu katika kufanya maamuzi au kutokuwepo mafundi, wahandisi na zana zenye kukidhi viwango.

Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara ya Muleba, Kanyambozo na Rubuja. Kwa niaba ya wananchi wa Wilaya ya Muleba kupitia Bunge lako nitoe shukrani kwa Mheshimiwa Rais na Wizara husika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wakati wa kutoa pole kwa wahanga wa tetemeko Mkoani Kagera Mheshimiwa Rais Dkt.. John Pombe Magufuli, alisikia ombi la wananchi na kuagiza kuanza ujenzi wa barabara ya Muleba Kanyamaboga – Rubya Hospital. Ni maoni yetu kuwa kiasi cha fedha kilichopangwa kwenye Bajeti ya 2017/2018 zitatolewa kwa wakati na mradi utatekelezwa. Aidha, ni mombi yetu kuwa usimamizi makini ufanyike ili tupate ufanisi wa hali ya juu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.