Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Shally Josepha Raymond

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. SHALLY J. RAYMOND: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Rejea ukurasa wa 148 wa Hotuba ya Mheshimiwa Waziri. Barabara ya Marangu – Tarakea, Rongai, Kamwanga - Bomang’ombe – Sanya Juu (kilomita 171); kwenye kila kifungu 259, mwisho wa paragraph; kuhusu kazi nyingine za kuanza ujenzi kwa kiwango cha lami barabara ya Kiboriloni – Tsuduni – Kidia (kilomita 10. 8).

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujua kipaumbele hicho kimetengewa shilingi ngapi na ni lini Ujenzi huo utaanza? Wananchi wanasubiri kwa hamu sana sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na yaliyo kwenye Hotuba ya Mheshimiwa Waziri, kuwa barabara ambazo Mheshimiwa Rais alipokuwa Njombe, alitoa ahadi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Moshi Vijijini, barabara ya RAU –Shimbwe juu kilometa 10; Vunjo – Barabara ya Himo – Mandaka, Kilema Maua.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na kukumbushia ahadi hizo naomba pia kukumbushia madeni ya Contractor wa Kichina aliyejenga Barabara ya Dumila – Kilosa ambaye alitulilia sana Kamati ya PAC tulipawatembelea. Kwa umoja wetu tuliona kuwa kusitishwa kwa Ujenzi ni gharama kubwa kwa Serikali. Ref. (Interest accumulation). Ushauri wangu kwa siku za baadaye, tujenge miradi michache na tuimalize kwa wakati.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho lakini si kwa umuhimu, nampongeza sana Mheshimiwa Waziri, Naibu Waziri, Katibu Mkuu na Watendaji wote wa Wizara kwa Hotuba nzuri na kazi nzuri pia, keep it up engineers.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja kwa asilimia mia moja.