Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Hussein Nassor Amar

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nyang'hwale

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. HUSSEIN N. AMAR: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza napenda kumpongeza Mheshimiwa Waziri na Naibu Waziri kwa hotuba yao nzuri sana. Pia naipongeza Serikali kwa kutimiza baadhi ya ahadi zake, hasa kwenye miundombinu ya barabara. Kwa Wilaya ya Nyang’hwale kuna barabara mbili za TANROADs, moja inayotoka Wilaya ya Geita – Nyang’hwale na ya pili inayotoka Busisi – Sengerema – Nyang’hwale – Kahama hizi zina hali nzuri kwa sababu zina matengenezo ya kila mara.

Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kukumbusha kwamba kuna ahadi ambazo ziliahidiwa katika Kampeni ya Mheshimiwa Rais wa Awamu ya Nne mwaka 2010. Katika ahadi hizo ni pamoja na kuijenga barabara ya kutoka Kahama - Nyang’holongo – Bukwimba – Karumwa – Nyijundu
– Busolwa – Ngoma – Busisi Wilayani Sengerema; kwa kiwango cha Lami. Kifupi kutoka Kahama – Nyang’hwale – Sengerema.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia Mheshimiwa Rais wa Awamu ya Tano alipokuja kujinadi katika Jimbo la Nyang’hwale aliahidi pia kujenga barabara hiyo kwa kiwango cha lami Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza; napenda kujua, je ni lini upembuzi yakinifu utaanza na kukamilika? Swali la pili; je ni lini ujenzi wa barabara hiyo utaanza na kukamilika?

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.