Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Prof. Jumanne Abdallah Maghembe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mwanga

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. PROF. JUMANNE A. MAGHEMBE: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza napenda kumpongeza Mheshimiwa Profesa Makame Mbarawa kwa hotuba nzuri ya Bajeti. Aidha, hotuba hii nzuri inatokana na kazi nzuri ya timu hii mahiri ya Wizara hii inayojumuisha Waziri, Naibu Waziri, Makatibu Wakuu na Wafanyakazi wa Wizara na Mashirika yote.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mkoa wetu wa Kilimanjaro una majimbo ya uchaguzi tisa. Kati ya hayo majimbo mawili tu ndiyo ya Chama Tawala cha CCM na yaliyobaki saba yako chini ya Chama cha Upinzani cha CHADEMA. Kwa bahati mbaya majimbo yanayoongozwa na CCM yalikuwa hayapewi fedha za utengenezaji wa barabara. Fedha karibu zote za kutengenezea barabara zinapangwa kutengeneza barabara katika Majimbo yanaongozwa na Upinzani. Msemo wa Wananchi wa Kilimanjaro umekuwa, kama mnataka barabara zenu zitengenezwe muwe chini ya CHADEMA. Napenda sasa nichukue fursa hii kuishukuru Serikali na hasa Wizara ya Ujenzi kuwa Bajeti ya mwaka huu 2017/2018 imejibu kilio cha wananchi wa Mwanga kwa kutenga fedha kuhudumia barabara ya Mwanga – Kikweni – Lomwe na Vuchama – Ngofi. Tuna imani kubwa kuwa hatua hii itasaidia sana kuleta imani ya wananchi wa Mwanga kwa Serikali yao na Chama chao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hatua zilizochukuliwa sasa zinatekeleza ahadi za Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano aliyetembelea barabara hii mwaka 2015 akiwa Waziri wa Ujenzi. Hivyo napenda kwa niaba ya wananchi wa Mwanga kumshukuru sana Mheshimiwa Rais.