Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Eng. Stella Martin Manyanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nyasa

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. ENG. STELLA M. MANYANYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kuishukuru Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, chini ya uongozi wake Mheshimiwa Profesa Mbarawa. Pia nampongeza Naibu Waziri Mheshimiwa Engineer E. Ngonyani kwa namna wanavyoshirikiana na Waziri wake. Nawapongeza Watendaji wote Wakuu wa Wizara hii na bila kumsahau Kaimu Meneja wa TANROADS Ruvuma Ndugu Razaq kwa kazi kubwa anayofanya hususan katika Jimbo langu la Nyasa ambalo lina changamoto kubwa sana ya miundombinu ya barabara.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimeona barabara ya Mbinga – Mbamba Bay ikiwa kwenye mpango wa kujengwa kwa kiwango cha lami. Barabara hii imo katika ahadi za Mheshimiwa Rais, siku anaomba kura alisema itajengwa kuanzia mwezi Aprili, 2016. Naomba sana ijengwe. Vile vile barabara ya Kitai – Lituhi na Lituhi – Mbamba Bay ambazo zilikuwa zimefanyiwa upembuzi yakinifu, sijui zimefikia wapi?

Vilevile nashauri barabara hiyo ichukuliwe ni Chiwindi (mpakani na Msumbiji) – Mbamba Bay - Lituhi badala ya Mbamba Bay - Lituhi kutokana na unyeti wake kuwa ni barabara ya mpakani na pia yenye fursa za utalii wa fukwe za Ziwa Nyasa. Hali kadhalika, naomba kuanza upembuzi wa barabara ya Kingirikiti hadi Liparamba - Mitomoni na kuunganishwa na daraja kuvuka Mkenda.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Waziri aliahidi kusaidiwa kujenga daraja baada ya vifo vya waliozama na boti Mto Ruvuma, kwenye bajeti hii, sijaona chochote! Tumeshawasahau wale watu tisa waliokufa. Mto ule hauna kivuko chochote cha uhakika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naungana na Mheshimiwa Jenista Mhagama barabara ya Likuyu Fuso - Mkenda inayounganisha na Msumbiji. Jimbo la Nyasa pia tutanufaika na barabara hii endapo itajengwa kwa kiwango cha lami, pamoja daraja la Mto Ruvu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vile vile niliomba kupandishwa hadhi barabara ya Chemeni - Kipapa Matuta – Mengo - Kihagara hadi Bandari ya Njambe kuwa ya TANROADS au Trunk road kwani inakidhi vigezo; pia imeunganisha fursa za kiuchumi kwa Jimbo la Nyasa na Mbinga Vijijini. Vile vile kupandisha hadhi kipande cha barabara ya Mpepo hadi Darpori.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nizidi kumshukuru Mheshimiwa Waziri kwa kukamilisha ujenzi wa meli mbili na hiyo ya abiria zinazoendelea kujengwa, pamoja na Bandari ya Ndumbi na Daraja la Mtu Ruhuhu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha.