Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Rev. Dr. Getrude Pangalile Rwakatare

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. DKT. GERTRUDE P. RWAKATARE: Mheshimiwa
Mwenyekiti, niungane na wenzangu wengi kwa kumpongeza Rais wetu Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, kwa uongozi wake mzuri. Naomba nimpongeze kwa kipekee Waziri wa Ujenzi na wasaidizi wake wote kwa hotuba nzuri na kazi nzuri wanayoifanya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana kwa juhudi za Mheshimiwa Rais wetu kutuletea Ndege mbili jumlisha nne, jumla yake sita. Hii imeturahisishia usafiri mikoani na imetuondolea aibu Kitaifa, nasi tuna ndege.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana kwa ujenzi wa daraja la Kilombero, limekamilika na limekuwa kiunganishi kati ya Wilaya ya Kilombero na Ulanga. Ni ukombozi mkubwa, Tunampongeza Mheshimiwa Rais wetu na Mheshimiwa Waziri na timu yake. Ahsanteni sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kuona barabara ya Kidatu – Ifakara – Malinyi –Songea; Ifakara – Kihansi Road zote ziko ndani ya Bajeti ya 2017/2018 na Dumila – Kilosa – Mikumi, kweli mnachapa kazi Mheshimiwa Mwenyekiti, nawaombea Mungu awape uwezo na afya mfanikiwe, Mungu aibariki Wizara ya Ujenzi, Waziri wake na timu nzima. Amina.