Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Elias John Kwandikwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. ELIAS J. KWANDIKWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze kwa kuunga mkono hoja. Naomba kuchangia mambo yafuatayo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza, ahadi ya Rais, ujenzi wa barabara ya lami. Wakati wa kampeni Rais, Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli aliahidi ujenzi wa barabara ya lami kilometa 10 Ushetu. Je, barabara hii itajengwa lini ukizingatia Jimbo la Ushetu halina barabara hata mita moja? Zaidi kuna vumbi jingi sana Makao Makuu ya Halmashauri ya Ushetu. Naomba Serikali itilie mkazo ujenzi wa barabara kama Mheshimiwa Rais alivyoahidi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pili, ujenzi wa minara ya mawasiliano. Halmashauri yetu ni mpya, tumefanikiwa kuwa na Wilaya ya Kipolisi, tumehamia Makao Makuu ya Halmashauri ya Wilaya, Kijiji cha Nyamilangano, Kata ya Nyamilangano. Mawasiliano ni hafifu na tunapata shida kubwa sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mawasiliano ya TEHAMA yanakwama ikiwemo mfumo wa malipo na mifumo mingine ya Halmashauri ya Wilaya yetu. Inalazimika wakati mwingine kazi zifanyikie kwenye Halmashauri huko Mjini Kahama.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mawasiliano ya kudhibiti usalama kwa Jeshi letu la Polisi pamoja na ulinzi shirikishi; niliwahi kuwa na swali nikaomba Kata za Nyamilangano, Uyogo, Chona, Ushetu na Kata nyingine, Serikali itusaidie tupate minara ili tukimbizane na maendeleo katika Jimbo la Ushetu. Naomba sana priority iwe Makao Makuu, yaani Kijiji cha Nyamilangano.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tatu, kupandisha hadhi barabara; tumekuwa na maombi ya kupandishiwa barabara hadi ya TANROAD barabara zinazounganisha mikoa hususani:-

(i) Barabara ya kutoka Tulelo - Mhulidede - Tabora kilometa 21. Barabara hii inaunganisha Mkoa wa Shinyanga na Tabora.

(ii) Barabara ya Chambo hadi Mambari. Barabara hii inaunganisha Mkoa wa Shinyanga hadi Tabora.

(iii) Barabara ya Masumbwe (Mbongwe – Geita), Mwabomba, Ulowa, Kaliua (Tabora). Barabara hii inaunganisha Mkoa wa Geita, Shinyanga hadi Tabora.

Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara hizi ni muhimu kwani maeneo haya yatachochea utalii, tutasafirisha mazao ya chakula na biashara na mambo mengi ya maendeleo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nne, kuhuisha Kamusi ya Barabara; naomba sana Wizara hii ihuishe Kamusi ya Barabara kwani inatunyima fursa ya kugawanya rasilimali vizuri. Mfano, Kamusi inayotumika, inaonyesha Ushetu ina mtandao wa barabara wa kilometa 416 tu wakati hali halisi tuna mtandao wa barabara kilometa 1,600. Tunaomba Serikali iboreshe Kamusi ya Barabara ili tushughulikie barabara na kupewa rasilimali kwa mtawanyiko ulio mzuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho naomba mambo hayo manne yashughulikiwe. Ahsante na naunga mkono hoja.