Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Daniel Nicodemus Nsanzugwako

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kasulu Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. DANIEL N. NSANZUGWANKO: Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba Serikali kuzingatia mambo muhimu yafuatayo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu ujenzi wa Reli ya Kati; Dar es Salaam – Kigoma ndiyo Reli ya Kati. Matawi yake ni Tabora – Mwanza; Kaliua – Mpanda - Kasanga Port, Uvinza - Msongati (Burundi) na Isaka - Keza. Uchumi wa reli na hasa reli ya standard gauge ni kubeba mzigo mzito, siyo kubeba samaki wala abiria.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tafadhali dhamira ya ujenzi wa reli ya kati izingatie msingi wa uchumi. Mzigo zaidi ya tani milioni 40 zipo nchi jirani ya DRC na zaidi ya mzigo tani milioni 10 zipo kwenye deposit ya Msongati katika Province ya Kusini Mashariki mwa Burundi. Mzigo upo DRC na sasa Burundi; na njia rahisi ya kwenda bandarini ipo kupitia Kigoma
- Dar es Slaam. Economic of Geography zizingatiwe. Matawi yaliyobaki ya Tabora/Mwanza na Isaka –Keza yasubiri! Iwe Second lot.

Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara ya Kidahwe – Kasulu - Kikondo na Nyakanazi, speed ya ujenzi wake inatia shaka sana. Kipande cha kilometa 50 cha Kidahwe - Nyumbigwa kimetumia sasa miaka saba. Naomba sana Serikali iharakishe ujenzi huo. Aidha, kutoka Nyumbigwa hadi Kasulu Mjini ni kilometa 9 - 10 hivi. Nashauri Mkandarasi aongezewe hizo kilometa 9 - 10 ili barabara hiyo ifike Kasulu Mjini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara ya Manyovu – Kasulu – Kibondo – Kabingo, usanifu wake na ujenzi wake unaanza lini? Tusubiri kwa miaka mingapi? Ishirini tena ijayo!

Mheshimiwa Mwenyekiti, Taarifa ya Kamati inaonesha Shirika letu la ATCL siyo mwanachama wa AITA. Je, taarifa hizi ni za kweli? Kama ni kweli, nini maana yake hasa kiusalama?

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba ushauri uzingatiwe na Serikali itoe majibu yaliyo sahihi.