Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Selemani Said Bungara

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Kilwa Kusini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. SELEMANI S. BUNGARA: Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote namshukuru Mwenyezi Mungu mwingi wa rehema na mwingi wa huruma.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahadi ya Rais katika Serikali ya Awamu ya Nne, Mheshimiwa Dkt. Kikwete aliahidi kujenga barabara ya Singino (Kwamkocho) - Kivinje ya urefu wa kilometa 4.2, barabara hiyo inaelekea katika Hospitali ya Wilaya. Ahadi hiyo ilitolewa na Mheshimiwa Rais wa Awamu ya Nne kwa umuhimu wa barabara hiyo ya kiwango cha lami, lakini kwa bahati mbaya mpaka leo, hiyo barabara ni tatizo. Katika bajeti ya 2016/2017, ilipitishiwa sh. 800,000,000/= kwa ajili ya kumalizia barabara hiyo lakini hadi leo hakuna kilichopatikana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Rais, Dkt. Magufuli, mwaka huu wakati alipotutembelea nilitoa kilio changu hiki cha barabara ya kiwango cha lami katika Hosopitali ya Wilaya. Alimwagiza Meneja wa TANROAD Mkoa wa Lindi amalize kero hii ya muda mrefu. Kwa heshima na taadhima naomba fedha ya bajeti ya 2016/2017, sh. 800,000,000/= zipatikane ili mradi huu wa barabara muhimu ya Kwamkocho - Kivinje ikamilike.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunamwomba Mheshimiwa Waziri, pia asimamie agizo la Mheshimiwa Rais wa Jamhuri Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Rais, Dkt. Magufuli aliyoagiza Nangurukuru kuwa Meneja wa TANROAD kuwa awasiliane na Wizara ili kero hii imalizike. Naomba kwa heshima na taadhima asimamie barabara hii muhimu kwa ajili ya faida ya kiuchumi na kijamii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hatujaona katika bajeti hii mwendelezo wa Uwanja wa Ndege na Bandari ya Kilwa Masoko. Naomba katika majumuisho ya Mheshimiwa Waziri anipatie taarifa ya Uwanja wa Ndege na Bandari.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba vile vile Mheshimiwa Waziri anifahamishe, malipo ya wananchi waliotathminiwa katika eneo la Uwanja wa Ndege. Katika majumuisho yake napenda kujua malipo ya wananchi hawa kwa muda sasa wa miaka mitatu hawajalipwa, ni lini watalipwa?

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho napenda kusisitiza:-

(a) Barabara ya Kwamkocho – Hospitali, ambayo ni ahadi ya Rais, Mheshimiwa Dkt. Kikwete.

(b) Bandari na uwanja wa ndege.

(c) Malipo ya wananchi waliotathminiwa katika eneo la Uwanja wa Ndege.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba ufafanuzi katika hizo kero zangu na naomba kuwasilisha.