Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, kipekee naomba nichukue fursa hii kukushukuru kwa kunipatia fursa nami niweze kuchangia katika hotuba iliyowasilishwa na Mheshimiwa Waziri. Naomba niungane na Wabunge wenzangu waliotangulia kumpongeza kwa kazi nzuri ambayo inafanyika, haihitaji ushahidi, kila mtu anaona kinachofanyika. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nijielekeze katika Jimbo langu. Kipekee nashukuru kwamba Serikali ina ujenzi wa barabara kwa kiwango cha lami kutoka Sumbawanga kwenda Kasanga Port na nimeona imetengwa jumla ya shilingi bilioni 74. Naiomba Serikali ihakikishe kwamba barabara hii inajengwa na ikamilike kwa wakati. Ni ukweli usiopingika kwamba mradi ukishachukua muda mrefu gharama yake inakuwa kubwa, lakini kama haitoshi kwenye hotuba ya Mheshimiwa Waziri nimeona kuna ujenzi wa barabara kwa kiwango cha lami kutoka Matai kwenda Kaseshe. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Waziri ni shahidi alikuja akatembelea barabara hii na akaahidi kwamba Kandarasi atapatikana na kazi hii itatolewa. Sasa naomba katika bajeti iliyotangulia ilikuwa imetengwa bilioni 11, safari hii imetengwa bilioni 4.9. Tafsiri yake nimesoma na kukuta kwamba Mkandarasi atapatikana muda wowote, kwa hiyo kiasi cha pesa tofauti ya bilioni 11 iliyokuwa imetengwa wakati ule na sasa hivi naamini itakuwa imetolewa na ujenzi wa barabara hii kwa kiwango cha lami utaanza mara moja. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine ambalo nimeliona ni vizuri nikampongeza Mheshimiwa Waziri, kwa mara ya kwanza kivuko cha Mto Kalambo kimetengewa pesa za kutosha milioni 100 kwa ajili ya usanifu. Naamini haitaishia katika usanifu, kazi ya kujenga kivuko kile itaanza kwani ni ahadi ya Mheshimiwa Rais alipokuja kuomba kura Kalambo na akaahidi kwamba yeyote ambaye hatahakikisha kivuko hiki kinajengwa basi ajiandae kupisha nafasi hiyo. Naamini Mheshimiwa Waziri bado anakumbuka, hiyo ni ahadi ya Mheshimiwa Rais ambayo haitakiwi kupingwa na mtu yeyote. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema kuhusu Jimbo langu, naomba niseme Kitaifa. Majuzi nilipata fursa ya kuuliza swali kuhusiana na suala la UDA Dar es Salaam na katika majibu ambayo nilipatiwa naomba nikwambie katika miradi ya kutolea mfano Kusini mwa Jangwa la Sahara yenye mafanikio ni pamoja na usafiri wa mabasi yaendayo kasi Dar es Salaam, lakini pamoja na treni ya umeme Lagos. Kwa Watanzania wengi tunadhani kwamba mradi huu ni mradi mdogo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nikuhakikishie ukienda duniani miongoni mwa miradi ambayo inasifiwa ni pamoja na usafiri wa mabasi yaendayo kasi Dar es Salaam. Ninachoomba ni vizuri Serikali ikahakikisha kwamba fursa hii inatolewa kwa Watanzania walio wengi ili hisa zile ambazo zinamilikiwa na Serikali zikaja kuuzwa kwa Watanzania walio wengi ili tukashiriki kumiliki uchumi huu kwa ajili ya Taifa la Tanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, wewe ni shahidi umekuwa ukipigia kelele kuhusiana na TTCL, naomba nikuhakikishie kama elimu ya kutosha haitolewi kwa Watanzania juu ya kununua hisa, basi hata hili ambalo umekuwa ukilipigia kelele kwamba Watanzania washirikishwe katika kumiliki halitawezekana. Mfano tunao, hisa ambazo zimetolewa kwa ajili ya kuuza za Vodacom imefikia tarehe 19 ambayo ilikuwa tarehe ya mwisho bado hisa hazijaweza kununuliwa. Naomba Wizara ya Fedha ichukue jukumu la kuhakikisha kwamba elimu kuhusiana na uwekezaji kwa maana ya kununua hisa inatolewa kwa Watanzania walio wengi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, wenzetu wa Kenya walivyokuwa wamepeleka hisa zao sokoni za Safaricom walikuwa wametoa kwa muda wa mwezi mzima lakini ndani ya siku kumi zile hisa zilikuwa zimeshanunuliwa kiasi kwamba wakalazimika wasitishe. Sasa kwa Watanzania imekuwa ni hadithi tofauti na kwa bahati mbaya sana unakuta wakati mwingine hata Wabunge pia hatuna elimu juu ya umiliki wa hisa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kwa makusudi Serikali lazima ihakikishe kwamba inatoa elimu maana taarifa ambazo tunapata kutoka kwa Gavana wa Benki Kuu ni kwamba…

T A A R I F A....
MWENYEKITI: Ahsante, ameshakaa. Mheshimiwa Kandege muda wako umekwisha. Hapana kengele ililia wakati wa taarifa.