Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Deogratias Francis Ngalawa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ludewa

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. DEOGRATIAS F. NGALAWA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuchangia. Kwanza kabla ya yote nipende tu kumshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, nipende kumshukuru Mheshimiwa Waziri na Naibu wake, pia na watendaji wote na viongozi wakuu wa taasisi ambazo zipo chini ya Wizara ya Ujenzi.

Mheshimiwa Naibu Spika, kitu cha kwanza ambacho pengine ningependa kuchangia leo ni juu ya mtandao wa mawasiliano ya simu. Ikumbukwe kando kando ya Ziwa Nyasa yaani Ziwa Nyasa lilivyo eneo kubwa ni eneo la Ludewa. Upande wa Nyasa kama Wilaya lina urefu wa kilometa 112 na upande wa Kyela lina urefu kama kilometa 10; lakini sisi Wana-Ludewa tuna kilometa zipatazo kama 220, cha kushangaza na cha kusikitisha, mpaka hivi ninavyoongea kando kando mwa Ziwa Nyasa tuna tarafa moja na tuna kata sita, hakuna kijiji wala Kata ambako kuna mawasiliano ya simu. Ikumbukwe kwamba eneo lile la ziwa lipo mpakani mwa nchi.

Mheshimiwa Naibu Spika, enzi zile sisi tukiwa watoto, yule bwana mkubwa akija unakuta kuna Sub Marine imesimama juu, wazee wetu walikuwa wanakimbia wanajifungia kwenye mahandaki, lakini mahandaki hayo sasa hivi hayapo. Kwa hiyo, eneo hili hata kama ni kutoa taarifa za kiulinzi na kiusalama tunashindwa. Kwa hiyo, nipende tu kumuomba Mheshimiwa Waziri alipe kipaumbele cha juu lile eneo kwa sababu ni eneo kubwa, kwa sababu ukiangalia ni kama vile tumetengwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, Nyasa yenye kilometa 112 vijiji vyake vyote vinamtandao wa mawasiliano, Kyela yenye kilometa kama 10 vijiji vyake vyote vina mtandao wa mawasiliano. Lakini unapoanza mipaka, beacons za Ludewa hakuna kijiji hata kimoja; vijiji 15, tukiweka kata sita vinakuwa vijiji 18 kata sita hakuna kijiji wala kata ambayo ina mawasiliano ya simu. Kwenye hili tunajiona kama ni wakiwa na kama vile tumetengwa. Ukija pia kwenye eneo hilo hilo la barabara yaani barabara zimeishia Nyasa na Kyela. Eneo la Ludewa halina kabisa. Tuna vijiji 15 ambavyo havijawahi kufika hata baiskeli, wananchi wameamua kuchimba wenyewe kwa mkono. Kwa hiyo, tunaiomba sasa Serikali ije iwaunge mkono wananchi wale ili waweze kupata barabara.

Mheshimiwa Naibu Spika, leo hii hata nikizungumzia suala la road upgrading Ludewa imeachwa kabisa. Kuna upgrading Makete kama mkoa, kuna upgrading Makambako, Wanging’ombe na Njombe lakini Ludewa imeachwa. Sasa huwa tunashindwa kujua Ludewa ina matatizo gani mpaka tusi-upgrade barabara hata moja? Mimi nipende kutoa masikitiko ya Wana-Ludewa kwa sababu inakuwa sio jambo jema.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuna maeneo ndani ya mkoa yanafanyia road opening, paving way, lakini eneo la Ziwa Nyasa ambalo lipo mpakani mwa nchi; hata kipindi kile wakati wale jamaa wanakuja kuja na ule mtafaruku tukawa tunashindwa wapi pa kwenda, barabara sehemu ya kukimbilia hatuna, mawasiliano kusema kwamba tutatoa taarifa kwenye vyombo vya usalama hakuna. Sasa nipende tu kujua labla pengine Mheshimiwa Waziri utakapokuja kuhitimisha utatuambia inawezekana Ludewa ina makosa ambayo imeifanya ndani ya Serikali hii.

Mheshimiwa Naibu Spika, tunakuja upande wa bandari. Tunaishukuru Serikali kwa zile meli tatu, meli mbili za mizigo na meli moja ya abiria. Vilevile kuna ujenzi wa gati ndani ya Ziwa Nyasa bado tunakuja kuona hapo hapo, upande wa Wilaya ya Nyasa kuna gati zinajengwa na kwenye bajeti mmeweka, upande wa Kyela kuna gati zinajengwa lakini ni upande wa Ludewa tu pekee yake ndiko hakuna gati.

Mheshimiwa Naibu Spika, bado tunakuja tunajiuliza maswali mengi sana, Ludewa ina tatizo gani na nchi hii? Kyela wanawekewa gati, Nyasa inawekewa gati. Halafu mahali huku ndiko ambako tunasema leo tuna uchumi wa viwanda. Tunapozungumzia uchumi wa viwanda huwezi ukaisahau Liganga na Mchuchuma. Liganga na Mchuchuma inakuja lakini miundombinu hakuna.

Mheshimiwa Naibu Spika, hebu angalia upande wa barabara; tunashukuru barabara ya Itoni - Njombe - Manda - Ludewa, mkandarasi yupo, ipo kwenye mobilization finalization, lakini kuna zile barabara ambazo ndio zinakwenda kwenye ile miradi, kuna barabara ya Mkiu kuelekea Madaba.

Mheshimiwa Naibu Spika, leo hii tunaambiwa inafanyia rehabilitation, lakini mimi nilikuwa najua tungeiweka sasa kwenye upembuzi yakinifu baadae iende kwenye usanifu wa kina ili twende kwenye lami, kwa sababu barabara hii ndiyo inayoelekea kwenye mradi mkubwa wa Liganga. Kwa sababu utakuta sasa miundombinu Ludewa ni miundombinu ya kizamani na hakuna consideration ambayo inafanyika kwa ujio wa miradi mikubwa kama ya Liganga na Mchuchuma. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa unaponiambia kwamba kuna flagship project za Liganga na Mchuchuma; na ndiyo maana huwa tunauliza, hii Liganga na Mchuchuma itaanza lini? Maana tungeweza kupewa schedule kwamba mwaka huu mpaka mwaka huu kuna hiki kuna fidia inafanyika, mwaka huu mpaka mwaka huu kuna hiki kinafanyika then baada ya hapo tunajua sasa mradi una- takeoff. Kwa inawezekana tunaona kwamba hata hii miundombinu inakuwa haiwekwi kwa sababu hata huo mradi wenyewe haufahamiki utaanza lini? Kama ungekuwa unafahamika utaanza lini mimi ni naamini kwamba hizi barabara zingeanzwa kutengenezwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sababau Nchi inavyoelekea kwenye viwanda mnakitegema chuma cha Liganga, Nchi inavyoelekea kwenye viwanda mnakitegemea umeme utakaozalishwa Mchuchuma, megawati 600; lakini kwa nini leo hatuweki hiyo miundombinu?. Wenzetu wote ambao wako ndani ya Mkoa kuna activities zinafanyika lakini ni Ludewa tu. Ukija gati inafanyika Nyasa na Kyela; Ludewa inaacha, ukija mawasiliano ya simu kuna Nyasa na Kyela; Ludewa inaachwa. Ukija barabara zinaishia kwenye beacon ya Kyela na huku inaishia kwenye beacon ya Nyasa lakini Ludewa inaachwa. Sasa lazima tujiulize panashida gani na Ludewa?

T A A R I F A...

MHE. DEOGRATIAS F. NGALAWA: Hiyo taarifa siipokei, kwa sababu haiwezekani watu wengine wanapewa fursa wengine hawapewi halafu uniambie kwamba… tena unanifundisha hata namna ya kusema, haiwezekani, tunazungumza vitu vilivyo-live. Mimi bajeti ninayo kila kitu kipo humu wakati mwingine mnaaweza mkaenda mbali labda kwingine labda pengine huku kwa sababu kuna Mawaziri na Ludewa hayupo Waziri, ndiyo mnataka kuniambia hicho, kwa nini Ludewa isipewe? Hiyo ndio hoja yangu mimi ya msingi

T A A R I F A...

MHE. DEOGRATIAS F. NGALAWA: Mheshimiwa Naibu Spika, hiyo taarifa siipokei. Mimi naongea kwa niaba ya wananchi wa Ludewa na wananchi wa hii. (Makofi)

Kwa hiyo, kama sehemu kipo na wakati huo mahitaji yetu yanalingana naona ni kama tunabaguliwa. Kwa sababu katika eneo la Ziwa Nyasa sisi ndio wenye eneo kubwa kuliko Nyasa, kuliko Kyela, sasa kule kuna kitu gani kikubwa ambacho hiyo miundombinu inapewa kipaumbele kuliko huku kwingine, kwa nini? Maana ukiniambia unajenga chuo lakini barabara hamna chuo hicho kitakuwa hakina maana yoyote. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo lazima ifike mahali kwamba hizi fursa lazima tupewe wote sawa. Kama ni chuo hata Nyasa kinajengwa, kipo kwenye programu, kwa hiyo, maana yake utakuwa una barabara, una gati na hicho chuo kitakuja. Ndiyo maana tunazungumza hapa Ludewa ina tatizo gani? Kama ni uvuvi, uvuvi mkubwa unafanyika Ludewa kuliko Nyasa na Kyela, wao wanajua, sisi ndio mabingwa wa kuvua, mabingwa wakuvua ni Wakisi kuliko Wamatengo, kuliko Wanyakuysa, sisi ndio tunaowafundisha, tumeenea kwenye mabwawa yote ya Tanzania. Ndiyo maana tunazungumza, kwa nini hatupewi kipaumbele? (Kicheko/ Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ndugu yangu Mheshimiwa Marehemu Deo Filikunjombe, Mungu amuweke mahali pema, amekuja hapa, amezungumza sana juu ya haya mambo; kapita kaenda. Ndiyo kwa maana sisi tunasema kwamba tunakosa gani? Licha ya kwamba tumekuwa tukiwasiliana na Waheshimiwa Mawaziri juu ya masuala haya. Si kwamba ni mara yangu ya kwanza mimi kuzungumza hapa Bungeni, nimezungumza sana na Mheshimiwa Mbarawa, ni mezungumza sana tu na Mheshimiwa Ngonyani, na inafikia kipindi hata Katibu Mkuu nimejaribu kuwa nampigia simu amekuwa hapokei, na mpaka nikajitambulisha naitwa Deo Ngalawa, Mbunge wa Ludewa still yet hapokei! Inawezekana Ludewa kuna matatizo. Ndiyo maana tunazungumza hilo.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo kama ni suala la fursa basi tupewe fursa sawa. Leo hii Ludewa barabara hazipitiki, hii barabara tunayozungumza ya Mkiu – Madaba imekata, watu wanakaa siku mbili njiani why, wakati wenzetu wanapeta? Vijiji havijawahi kufika baiskeli hata siku moja, pikipiki haijawahi kufika vijiji 15. Wananchi wameamua wenyewe kuchimba, kwa nini Serikali isije? (Makofi)

Tumeamua wenyewe clips za wananchi kuchimba Mheshimiwa Waziri pamoja na Mheshimiwa Naibu Waziri niliwaonesha kwamba tumeamua kuchimba wenyewe kwa majembe kwa nyundo kwa mitalimbo. Leo hii tunapokuja kuzungumza unasema tusilinganishe, tusilinganishe kwa base ipi? Ifike mahali fursa lazima tupewe sawa, mimi langu ilikuwa ni…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

HE. DEOGRATIAS F. NGALAWA …kufikisha ujumbe huo na naunga mkono hoja.