Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Bhagwanji Maganlal Meisuria

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chwaka

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. BHAGWANJI MAGANLAL MEISURIA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante umenipa nafasi Mungu akuweke, nakupongeza sana. Naipongeza Kamati yangu ya Miundombinu, Mheshimiwa Mwenyekiti pamoja na Wajumbe wote wa Kamati yangu, kwa sababu tumetembea katika maeneo mbalimbali na nimefaidika, na sisi tumeona eneo lingine jipya. Vilevile Rais wangu Mheshimiwa John Pombe Magufuli amefanya kazi nzuri sana katika Tanzania yetu, Mungu amuweke maana yake ana mbinu ya Rais wetu Mheshimiwa Narendra Modi wa India, yaani Narendra Modi anafanya mambo yake na yeye anachukua mbinu hiyo hiyo, Mungu amsaidie. (Makofi/Kicheko)
Mheshimiwa Naibu Spika, nampongeza Waziri wangu wa Miundombinu, Naibu Waziri, pamoja na watendaji wake wanafanya kazi nzuri pamoja ofisi yake wanafanya kazi nzuri wanamsaidia sana, Mungu amuweke.
Mheshimiwa Naibu Spika, tunakuja katika mada yetu inayohusu Mkongo wa Taifa (Data Centre) yaani mitandao ya simu. Kamati yetu tumekwenda juzi kutembelea, nimeona mambo mazuri kabisa, yaani hiyo mitandao chini kwa chini (underground) imekuja kutoka India, South Africa na Zambia mpaka hapa Dar es Salaam, tumeona mitandao hiyo, nampongeza Mheshimiwa Rais wetu Magufuli, amefanya mambo hayo, yaani nchi nyingine hakuna lakini hapa Tanzania ipo. Mitandao hiyo imegusa Dar es Salaam, Zanzibar lakini wale watu ambao ni washirika wa mtandao huo, Zantel, Airtel Tigo pamoja TTCL wamefanya mambo mazuri sana. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, imetengeneza database ili hawa watu wa mitandao, wale wa Zantel na wengine wanunue hiyo data waje kutia katika mitandao yetu katika database. Kampuni hizo waje watie katika biashara yetu katika database, yaani wao wasitumie yao watumie ya Tanzania, ili sisi tupate pesa. Mheshimiwa Magufuli amefanya mengi pamoja na Rais wetu wa zamani Mheshimiwa Jakaya Kikwete safi yaani wamefanya vitu vya kuleta baraka na Tanzania yetu tushinde. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, tunakuja katika barabara, tumetembelea barabara nyingi sana na juzi tumetembelea barabara ambayo Mheshimiwa Rais amefanya kuwa barabara kubwa, ina watu wengi, amekatisha sasa, ameipeleka barabara hiyo mpaka Kiwanda cha Saruji cha Wazo pale. Halafu kutoka pale inakwenda moja moja mpaka bandari, inakwena uwanja wa ndege, amegawa sehemu mbalimbali, mjini pamoja na huko sehemu za Dar es Salaam. Barabara hiyo ina watu na magari mengi, kwa hivyo nampongeza Mheshimiwa Rais wangu Magufuli. Mimi naomba Rais wangu Mheshimiwa Magufuli asaidie kidogo barabara za Zanzibar. Uwezo wetu ni mdogo, lakini mimi naomba Mheshimiwa Rais wetu wa Muungano aisaidie Zanzibar ili na sisi barabara zetu ziboreshwe.
Mheshimiwa Naibu Spika, tunakuja uwanja wa ndege. Kweli mimi nampongeza Mheshimiwa Rais amefanya maboresho mengi sana, ameleta ndege kubwa. Tunaona uwanja wa ndege wa Dar es Salaam umeboreshwa vizuri kabisa. Sisi tulikwenda kutembelea Terminal B, tumeona mambo mazuri, yaani watalii watakuja wengi sana. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini vilevile naomba Serikali iboreshe uwanja wa ndege wa Zanzibar, sisi wote ni wa Muungano, ndugu mmoja hatuna ubaguzi, uwanja wetu wa Zanzibar na sisi tuuboreshe kwa sababu terminal ipo na wanakuja watalii pesa zote zinaingia Tanzania tutaondosha umaskini wetu. Vilevile viwanja vya ndege vidogo vidogo Tabora, Mwanza, Moshi, Kilimanjaro jamani hivi viwanja vya ndege kama sisi wananchi tuvitumie tunaongeza mapato, tunaongeza vitu mbalimbali, tutaondosha umaskini, tunatafuta mapato tunaleta maendeleo.
Mheshimiwa Naibu Spika, umenipa nafasi nakushukuru sana Mungu akuweke. Tunakuja katika bandari na bandari yetu imeboreshwa na tumekwenda kutembea bandari ya Dar es Salaam, tunataka kupanua bandari, na kupanua kwake kwa sababu zitapita meli mbili pamoja. Mimi nampongeza Mwenyekiti wangu wa Kamati, yaani mimi pia nimefaidika kwa kuingia ndani ya Bunge nafahamu nini maana ya Muungano na nini ni Serikali. Kumbe Serikali iko imara, na Marais wa awamu zote wamefanya kazi ya kuleta maendeleo katika nchi yetu kwa kuondoa umaskini wetu. Nampongeza na Mwenyezi Mungu aipe nchi yetu ya Tanzania ipate baraka na kila kheri. (Kicheko/Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, bandari yetu ya Dar es Salaam tunapanua, lakini mimi ninaomba Serikali yetu vilevile, bandari ya Zanzibar tuko katika enzi yetu ya zamani, tunataka na sisi bandari yetu ya Zanzibar pia tuboreshe ili tupate kuweka makontena nyingi kuliko zile, ili pia watu mbalimbali waje. Vilevile mimi ninaiomba Serikali yangu, Waziri wangu, Rais wangu bandari ya Mwanza, Tabora,
Bagamoyo, Tanga umenifahamu paleā€¦
(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)
MHE. BHAGWANJI MAGANLAL MEISURIA: Mheshimiwa Naibu Spika, mimi naunga mkono hoja, ahsante sana.