Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Jaku Hashim Ayoub

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

House of Representatives

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. JAKU HASHIM AYOUB: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Bila kupoteza muda wala kurembaremba sana, kwanza nachukua fursa hii kumpongeza Mheshimiwa Waziri na baadhi ya watendaji wake, maana wengine siwajui kwa umakini wao na utendaji wao. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nichukue fursa hii kumsifia Mheshimiwa Waziri, ikiwa yeye ana pumzi zake, na mimi nina pumzi zangu. Watu wengi baada ya mtu kuondoka ndiyo humsifu mtu kwamba alikuwa mzuri; lakini namsifu nikiwa niko hai na yeye yuko hai.
Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Waziri ni miongoni mwa Mawaziri wa Dkt. John Pombe Magufuli aliyekuwa bora katika utendaji wake, bila kuficha! Mheshimiwa Waziri ni msikivu, utendaji wako tumekuwa tukiuona ambao hautaki torch. Ni Waziri unayeshindana kidogo na Mheshimiwa Waziri Mwigulu Nchemba, kwa muda mfupi amechukua Wizara mbili kuongoza na huo ni kutokana na umakini wako Mheshimimiwa Waziri. Waziri ambaye hana Jimbo, akitokea Ikulu mara nyingi. (Kicheko/Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, hii ni kutokana na elimu yake, utendaji wake, umakini wake na busara zake, ndiyo maana Marais wengi huvutiwa na wewe kutokana na umakini wako. Mheshimiwa kuna usemo usemao; mgema akisifiwa, tembo hutia maji, unatokea Zanzibar. Hata Mheshimiwa Kishimba anatamani kuwa Mzanzibari Mbunge wa Kahama, lakini Mungu hajamjalia. (Kicheko/Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nitaigusa Bandari ya Dar es Salaam na nitakuwa sijamtendea haki Mheshimiwa Dkt. Harrison George Mwakyembe kwa kazi aliyoifanya pale. Mabenki yale baada ya kuchangia kipindi cha mwaka uliopita, akafungua benki na tumeziona. Mheshimiwa Dr. Mwakyembe keep it up! (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba hapa, kidogo Mheshimiwa Waziri anisikilize kwa umakini kabisa; na ball pen iwe karibu kuandika; yatamgusa Engineer Kakoko wa bandari ile na Port Manager ambaye ana-act, Fredy John Liundi. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, hali ilivyo katika bandari ya Dar es Salaam bado kuna matatizo, kauli siyo nzuri na sisi Waislamu tunasema maneno mazuri ni sadaka au methali inayosema, kauli nzuri humtoa nyoka pangoni. Sasa Mheshimiwa Waziri anza kuandika mwanzo. Customer care kwanza haipo katika bandari ile. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, customer care katika bandari ile haipo. Mheshimiwa Kakoko siyo kila anayepepesuka ni mlevi. Kazi zote hizi Mheshimiwa Kakoko huwezi kuzifanya peke yako. Kama yupo juu, basi nafikiri utakuwa unasikia huko. Madaraka haya lazima mgawane na wenzio, utakuja kuumia, sisi bado tunakuhitaji. Huu ni ushauri wangu, bado tunakuhitaji. (Kicheko)
Mheshimiwa Naibu Spika, namwomba Mheshimiwa Waziri, ndungu yangu, trend ya mizigo ya miaka kumi au saba ya nyuma, mizigo iliyoingia na iliyotoka na sasa hivi, kaiangalie. Tuelezane ukweli, mizigo iliyoingia na kutoka imeshuka. Ni ushauri wangu. Kaangalie trend ile ya miaka saba au sita ya nyuma au mitano iliyotoka hivi sasa, utaona ukweli ulipo. Hali siyo nzuri kusema ukweli.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba ni declare interest, mimi ni mfanyabiashara, siwezi kudharau dafu kwa embe la msimu. Hii siasa kesho Mungu akijaalia haipo, lakini dafu siku zote unaweza kulipata. (Kicheko)
Mheshimiwa Naibu Spika, kuna VAT on transit hivi vitu wananchi wanalalamikia sana. Ajira mnavyotangaza, hivi juzi mmetangaza ajira, sijui kama mmezitangaza, lakini kuna watu mmewaajiri. Tuwe wawazi, tuwe wakweli katika bandari.
Mheshimiwa Naibu Spika, DG baadhi ya wafanyakazi wanamwogopa sasa hivi. Kama wanapita njia hii wafanyakazi wanamwogopa, wanapita njia nyingine. Liandike, ulifuatilie kama nasema ni ya kweli ama siyo ya kweli.
Mheshimiwa Naibu Spika, wafanyakazi wengine wanaomba muda wao wa kustaafu kabla haujafika, wanaogopa bandarini kutokana na matukio yanayotokea. Suala za wizi limekuwa wizi tu. Ndiyo yale niliyosema, siyo kila anayepepesuka ni mlevi. Muda wa kustaafu wafanyakazi haujafika, watu wanataka kustaafu kuondoka, wameshachoka. Tena wale wazoefu; tutakuja kutafua rasilimali hiyo wakati huo hatuna. Huu ni ushauri wangu, Mheshimiwa Waziri fuatilia niliyokwambia. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nije DMI (Chuo cha Baharia). Kuna eneo pale limekaa miaka nane au kumi, kibanda kimeshaanguka. Unafanya biashara; mimi mwenyewe binafsi nilishapeleka barua pale, lakini hakuna majibu, hakuna kilichofanyika. Nafikiri wenyewe wapo hapo. Imekuwa kama nyoka wa mdimu Mheshimiwa Waziri. Nyoka wa mdimu hukaa kwenye mdimu, yeye hana kazi nazo na ukienda kuchuma, anakurukia, faida iko wapi? Siyo kitu kizuri!
Kodi zingesaidia! Wengine wamekodishwa maeneo yale, wengine hawajakodishwa, wako kinyume na utaratibu.
Mheshimiwa Naibu Spika, nije katika Bandari ya Letakii, hapa pana dhambi na maonevu makubwa. Wafanyabiashara wa Zanzibar na Zanzibar tegemeo lake kubwa ni biashara. Leo viazi, cabbage, pilipili ina-megati nane inapekuliwa. Vipo hapa hapa, local food hiyo, hatutendi haki. Kama unataka, nitakutajia; kuna geti namba tatu Mheshimiwa Waziri. Malindi pana geti pale pale, mita 50 haijafika, pana mizani, halafu unakuta mizani yenyewe. Usumbufu, mnasema mnapunguza foleni, huku mnazidisha foleni. Umefunga mlango wa mbele wa nyumba wa nyuma umefungua.
Mheshimiwa Naibu Spika, watu wanalipa ada za bandari pale kwa muda mrefu, lakini charge zimekuwa nyingi. Bandari zimekuwa na mapote; ikija mvua tope, likija jua, vumbi; wafanyakazi wana mazingira magumu katika kazi ile. Nampongeza sana Acting Port Manager, John Liundi, kazi anayofanya pale nitakuwa sijamtendea haki na nitakuwa mtovu wa adabu wa mwisho kama sikumshukuru kwa mazingira ya kazi anayofanya pale. Hongera Port Manager unayekaimu kwa muda. Pengine Mungu atakujalia muda siyo mrefu utatoa fupa hili.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuna yule mlinzi pale anayeshughulikia ulinzi wa bandari. Kwa muda mrefu ulinzi umeimarika bandari ya Dar es Salaam. Tuwape haki zao. Mnyonge mnyongeni, haki yake mpeni. Jamaa wa pale anaitwa Twange, amefanya kazi nzuri ya ulinzi.
Mheshimiwa Naibu Spika, kabla muda haujamalizika, nije kwenye ndege, Bombardier sasa.
Mheshimiwa Waziri chukulia mfano Pemba kule Makombeni kuna mabonde ya mpunga, umelima, umeshaotesha mpunga wako, kuna ndege wanaitwa tongwa wale, ukishauacha unakuja kuuvuna. Hawa wana malalamiko.
Mheshimiwa Naibu Spika, umenunua baiskeli, leo unashindwa kununua pump tu kujaza upepo baiskeli! Hebu waingizeni pesa tusije tukawalaumu, baadaye tukawa tunasema Tanzania wanafanya vibaya. Wanahitaji mtaji hawa. Kama hamuwezi, wakopesheni five billion. Leo tunafanya vitu vizuri, baadaye tutakuja ku-fail.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuna mtu msikivu sana yule CO hata jina lake silijui mimi. Ni rasilimali kubwa sana yule. Maneno yake tu ukisikia akizungumza utafikiri asumini zinatoka mdomoni, harufu yake. Ndiyo yale walisema, maneno mazuri ni sadaka. Ongeza mtaji wa Mtanzania. Hawawezi kufanya kazi wale bila kuwa na mtaji. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kutoka hapo utaratibu wa Bombardier jamani, kuja usiku sisi kama walinzi tumechoka. Jaribuni kupanga utaratibu, Bunge linaanza Jumanne. Pangeni Jumatatu angalau saa 10.00 tuondoke kule. Badilisheni utaratibu huu. Halafu bei zake zikoje? Leo unanunua bei nyingine, kesho bei nyingine, kiti ndiyo kile kile. Hebu jaribuni kufanya utaratibu (format) mwingine. Bunge hapa linaanza Jumanne, Jumatatu angalau ndege ingeondoka saa 10.00 pale.
Hayo ni maoni yangu, nanyi kama hamtaki mtachangia. Kila mmoja ana uhuru wake wa kusema.
Nije kwa SUMATRA. Mheshimiwa Branch Manager, sheria hii inaumiza watu...
Mheshimiwa Branch Manager, sheria hii inaumiza (Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)