Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mpango wa Pili wa Maendeleo wa Taifa kwa kipindi cha Miaka Mitano kuanzia mwaka 2016/2017 – 2020/2021

Hon. Eng. Edwin Amandus Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Mpango wa Pili wa Maendeleo wa Taifa kwa kipindi cha Miaka Mitano kuanzia mwaka 2016/2017 – 2020/2021

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, awali ya yote naomba nimshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunipa fursa hii ya kuingia katika jengo hili kwa mara ya kwanza. Kupitia fursa hiyo naomba niwashukuru wapiga kura wote wa Jimbo la Namtumbo kwa kazi waliyoifanya pamoja na mateso yote ya kupiga kura mara tatu na mwisho nichukue fursa hii kumshukuru Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli kwa kunipa nafasi hii ya kuwatumikia Watanzania. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, Mpango wa Pili ni mwendelezo wa Mpango wa Kwanza pamoja na nyongeza inayozingatia dhima ya Serikali ya Awamu ya Tano kuijenga Tanzania ya viwanda. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, suala la miundombinu iliyopangwa katika Mpango wa Kwanza na hii iliyoongezeka katika Mpango wa Pili yote inahitajika na tutaihitaji katika mpango wa tatu. Kwa hiyo, hoja kwamba tulitekeleza asilimia 53 tu katika awamu ya kwanza ni kutokana na uwezo wetu, sasa tunaingia katika Mpango wa Pili tutamalizia asimilia 47 pamoja na nyongeza nyingi ambazo zipo katika Mpango huu wa Pili, ambao Mheshimiwa Dokta Mpango ameuleta na kwa kweli naomba nichukuwe fursa hii nimshukuru sana alikuwa amechelewa kuja nafasikatika hiyo!
Mheshimiwa Naibu Spika, wengi wameongelea umuhimu wa miundombinu, nashukuru sana Bunge zima limeungana katika kukubali Mpango, tunatofautiana katika utekelezaji, wapo wanaodhani utekelezaji hautafanyika na wapo wanaoomba tupate nguvu tutekeleze. Kwa maana nyingine Mpango wote tunaukubali, labda katika eneo moja tu ambalo Mheshimiwa Bashe ametoa maoni tofauti kwamba suala la kufufua Shirika letu la ATCL liangaliwe kwa namna tofauti kwa kuzingatia hasara zinazopatikana katika mashirika ya ndege duniani.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nimtoe wasiwasi Mheshimiwa Bashe na wengine wenye dhana kama yake, usafiri wa anga ni necessary evil kwa nchi yoyote, hatuwezi kuukwepa. Inawezekana from micro point of view kampuni ikapata hasara, lakini kama nchi usafiri huo unachangia katika sekta mbalimbali na overall sekta hiyo ya usafiri wa anga inatuletea faida kubwa, hatuwezi tukaiacha ikashikiliwa na wafanyabiashara peke yao, muda wowote wanaweza wakaondoka kwa sababu wao wanaangalia faida na wanaangalia faida katika kampuni yao peke yake, wakati sisi tunaangalia faida kwa mapana yake ni pamoja na mchango wake katika sekta ya utalii na masuala mengine. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, tumedhamiria, kujenga reli ya standard gauge ya Kati na matawi yake yote, ya Mtwara Corridor na ya Kaskazini. Dhamira hiyo kama ambavyo mtaiona katika bajeti inayokuja na mmeona katika kitabu cha Mheshimiwa Mpango, Waziri wa Fedha na Mipango, tumeshaonyesha kwa kutenga trilioni moja haijawahi tokea! Kwa hiyo, naomba mtuamini. Ninalo jembe linaloniongoza, linaloongoza Wizara hii, Profesa Makame Mnyaa Mbarawa. Kwa wale wanaomfahamu yale aliyoyafanya katika Wizara ya Mawasiliano, aliyafanya kimya kimya wanamfahamu ni mtu wa aina gani na mimi nashukuru kufanya kazi chini yake, kwa sababu naamini nitaweza kukidhi haja yangu ya kuwatumikia Watanzania kwa namna ambayo tutafika huku tunakokwenda, uchumi wa kati. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, tutatoka kwenye kusherehekea flyover na interchanges moja tutakuwa na flyovers na ma-interchanges nyingi sana.
NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Naibu Waziri Ngonyani muda wako umekwisha!
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Aah, ni kengele ya kwanza hiyo!
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuchukua fursa hii kuunga mkono kwa nguvu sana na kwa kutupendelea sisi watu wa miundombinu na hatutawaangusha.