Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hotuba ya Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakati wa Kufungua Bunge la Kumi na Moja

Hon. Peter Joseph Serukamba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigoma Kaskazini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Hotuba ya Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakati wa Kufungua Bunge la Kumi na Moja

MHE. PETER J. SERUKAMBA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa, nafasi na mimi niweze kuchangia Hotuba hii ya Mheshimiwa Rais. Kwanza naomba niwashukuru kwa dhati kabisa, wananchi wa Kigoma Kaskazini, kwa heshima kubwa waliyonipa, naweza kusema namuomba Mungu nisiweze kuwaangusha hata kidogo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili, hotuba ya Rais ni nzuri sana. Hakika hotuba ile ilikuwa inaonesha dira ya miaka mitano. Lakini pia baada ya hotuba ile Rais ameanza kutekeleza, wazungu wanasema, he is walking the talk, ameanza kutekeleza aliyoyasema tarehe 20 Novemba hapa Bungeni. Sasa unaanza kuona nchi ambayo inachukia rushwa kwa vitendo. Tunaanza kuona ahadi zetu zikitekelezwa, tunaanza kuona tukielekea kwenye nchi ile ya ahadi tuliyoitarajia. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, Rais anavyofanya kazi unaona Taifa letu likienda sasa kuanza kufanya kazi. Lakini wako wanazuoni wanasema, pamoja na yote, no gain without pain and this is leadership. Kwa hiyo, unaweza ukaona mambo yanavyokwenda, pain itakuwepo, lakini hatuwezi kufanikiwa bila kuwa na pain.
Mheshimiwa Rais ameongea mengi, mimi nitachangia machache la kwanza, maji. Mimi ninaamini kama kuna vita ya tatu ya dunia itatokea itasababishwa na maji. Tatizo la maji nchini ni kubwa sana, hasa katika Jimbo langu la Kigoma Kaskazini, Kata ya Kalinzi hatuna maji, Kata ya Mkigo hakuna maji, Kata ya Kagongo hakuna maji, Kata ya Ziwani hakuna maji, Kidahwe hakuna maji na Mayange hakuna maji. Lakini naomba nitumie nafasi hii kuishauri Serikali. Ukiangalia matatizo tunayokumbana nayo ya mazingira duniani, tunakoelekea mito mingi itaanza kukauka.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi ningeomba, niiombe Serikali ilifanya uamuzi mkubwa kutumia maji ya Lake victoria, lakini sisi tumebarikiwa tuna Lake Victoria, tuna Lake Tanganyika na tuna Lake Nyasa. Mimi ningeshauri Serikali, umefika wakati, waone umuhimu wa kutumia maziwa haya ili kuweza kupeleka maji katika maeneo mengi ya nchi yetu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine ni Sheria ya Ununuzi, Mheshimiwa Rais alisema, kama kuna sheria mbaya ni Sheria ya Ununuzi, na mimi nasema sheria ile ni mbaya sana, inatumia pesa nyingi sana kama walivyosema watu wengine. Tukipitisha Bajeti mwezi wa saba, inaanza kutumika Bajeti ya Serikali, Wizara zote zikianza kufanya manunuzi, mpaka mkandarasi anaingia kazini, siku anaanza kutangaza na hapo wameenda wamefata sheria ni miezi sita, haiwezekani! Kwa hiyo, ina maana tunatumia miezi sita yote tunafanya kazi za procurement. Halafu wakati wanataka kuanza kutekeleza mvua ni nyingi kubwa sana nchini, kwa watu wa barabara wanajua matokeo yake pale wanasimama, kwa hiyo tunamaliza mwaka, kwa kweli kazi nyingi hazijafanyika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, UN System wana kitu kinaitwa Universal Procurement List. Ningeomba nishauri Serikali umefika wakati na sisi tuandae Tanzania Procurement List. Maana yake nini, maana yake ni kwamba tunaenda kununua vitu vyote kwa supplier mwenyewe kwa manufacturer mwenyewe, tuta-serve pesa nyingi, tutapata vitu kwa bei ambayo ni ya chini, lakini na quality itakuwa ni kubwa. (Makofi)
Leo hii, hii habari ya list evaluated bidder, inafanya bei iwe kubwa, kalamu ya shilingi 1000 tunainunua kwa shilingi 5000, mtu amefuata sheria na tumeibiwa tunaangalia iko within the law, ningeiomba Serikali wailete sheria hii haraka sana.
Mheshimwa Mwenyekiti, lingine ni suala la PPP. Toka nimeingia Bungeni huu ni mwaka wa kumi naenda mwaka wa 15, tunaimba PPP, mpaka leo haijatekelezwa. Ningeomba niishauri Serikali, haiwezekani tukafanya maendeleo makubwa ya haraka kwa kutumia pesa za Serikali. Kama kuna mtu anadhani Serikali hii tunaweza tukafanya kwa pesa zetu wenyewe, ni tatizo kubwa. Na wenzetu we are not inviting the will, wenzetu wameanza.
Mheshimimiwa Mwenyekiti, ningeomba sana kwa mfano, reli, bandari, umeme, barabara, hasa barabara kubwa ya Dar es Salaam kwenda Arusha, Dar es Salaam kwenda Mwanza, Dar es Salaam kwenda Mbeya, kwa kweli kujenga barabara hizi kwa fedha zetu wenyewe hapana. Tuwape watu wajenge, waweke road toll, tutalipia, lakini tutapata barabara nzuri, na tutapunguza ajali. Wenzetu Malaysia wanafanya, South Africa wanafanya, sisi tatizo ni nini? Ningeomba Serikali walitatue tatizo hili.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika hili Tanzania tumebarikiwa sana. Tuna uchumi wa kijiografia, naombeni Serikali tumesema inatosha, tutumieni nafasi yetu ya kijiografia, Tanzania tuko well located kijiographia, Tanzania Mungu ametujalia kwa sababu ya Chama chetu kuna amani na utulifu, naombeni hii amani na utulivu iwe ni resorces ya kuleta maendeleo. Hatuwezi kuwa kila siku tunaimba, nchi yetu ni ya amani na utulivu, mambo hayaendi. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho katika hili, hatuwezi kuendelea bila private sector, niwaombe watu wa Serikali nimeanza kusikia sentiments za kuona wafanyabiashara wanatuibia, wafanya biashara ni watu wabaya, naombeni tuondoe hizi sentiments. Haziwezi kutupekeka popote, sungura wetu bado ni mdogo. Kama tunataka tuondoke hapa tulipo na wengine wote wamefanya lazima tuitumie private sector.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mifugo. Tanzania Mungu ametubariki, lakini laana hii ya mifugo haitusaidii sana, ndiyo maana tunauana kila siku kwa sababu ya mifugo, ningeomba mifugo hii tuitumie vizuri.
Mheshimiwa Mwenyekti, kilimo. Kilimo natamani ningekuwa na muda mrefu sana. Lakini itoshe kusema mwaka 2005 tulitumia bilioni 7.5 kwa ajili ya ruzuku, tukapata mazao ten million tones za mazao ya chakula. Mwaka 2015 tumetumia bilioni 299, tumepata mazao tani milioni kumi na sita. Ni investiment tunatupa bure. Ningeomba tumefika wakati twende kwenye commercial farming, tusiogope, haiwezekani kila mtu alime, haliko Taifa la namna hiyo. Tunaogopa commercial farming umefika wakati twende kwenye commercial farming, itatusaidia sana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho ni elimu. Naipongeza sana Serikali, inafanya kazi kubwa kwenye elimu bure, lakini mimi bado nina tatizo pamoja na elimu bure mimi nadhani umefika wakati tuunde Tume ya Elimu. Ili tuangalie matatizo yetu ya elimu, ipitie mfumo wetu wa elimu kuanzia vidudu mpaka university. Tuangalie watu wanaomaliza darasa la saba wameelimika? Wanaomaliza form four wameelimika? Wanaomaliza Chuo Kikuu wameelimika? Haiwezekani tutakuwa tuna-solve watu hawawezi kulipa school fees tuwatolee bure, vitabu tuwanunulie, bado hatujapata tatizo letu la mfumo wa elimu ni nini.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sisi siyo wa kwanza, Wamarekani mwaka 1981 wakati wa Rais Reagan waligundua mfumo wao wa elimu unashindwa duniani, wakaunda Commission ya Elimu. Watu wote mkaangalie, wakatoa ripoti mwaka 1983 inaitwa A Nation at Risk, waliona Taifa lao linaenda kwenye majanga. Kwa sababu tusipokuwa na elimu bora viwanda tunapiga story tu hapa. Kilimo tunapiga story, uvuvi tunapiga story, kama hatuja-solve tatizo la elimu na elimu watu wetu waelimike na you might have all the Professors lakini hawajaelimika!
Mheshimiwa Mwenyekiti, ningeomba sana niishauri Serikali umefika wakati tuuangalie upya mfumo wetu, na ndiyo maana anakuja Waziri wa Elimu leo analeta GPA, mwingine anakuja kesho anaondoa GPA, kwa sababu gani hatujui tatizo letu ni nini. Hatujui kwa nini watu wanafeli, kwa hiyo mimi ningeshauri Serikali, atakuja Ndalichako leo amesema turudi kwenye division, Ndalichako kesho anaondoka anakuja mwingine watu wanafeli sana anajenga hoja anadhani ndiyo solution tunarudi kule tulikotoka. Ni kwa sababu hatuja-diagnosis tatizo letu la elimu nchini.
Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hayo, naunga mkono speech ya Rais. Nampongeza Mheshimiwa Rais, tunamuombea kila la kheri, aendelee kufanya kazi, aendelee kutumbua majipu, ninaamini Watendaji wa Serikali sasa wataanza kutekeleza wajibu wao. (Makofi)