Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Katiba na Sheria

Hon. Mary Deo Muro

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Katiba na Sheria

MHE. MARY D. MURO: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuchangia kama ifuatavyo:-
Nishauri Serikali kuweka bayana mambo ya kisheria na kuyatendea haki mfano haki ya kujieleza, haki ya kupata habari, haki ya kuishi, ni vizuri Serikali ikatendea haki maeneo hayo ili taifa liwe na Amani.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naishauri Serikali itambue kuwa amani haiwezi kuwepo bila haki ambayo inatokana na utawala wa Sheria. Sheria za Ndoa na mirathi zipo lakini wananchi wa kawaida hawana elimu ya sheria. Pia nashauri Serikali kufanya juhudi ili kutoa elimu ya sheria kama ilivyo kwa matangazo mengine ya UKIMWI na madawa ya kulevya.
Nashauri Serikali kutembelea mahakama zetu zilivyo na wafanyakazi wanaoishi na kufanya kazi katika wakati mgumu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia nishauri kuhusu upelekaji wa wafungwa kutoka mahabusu imekuwa shida, hivyo Serikali iangalie kwa nini kutokana na ukosefu wa usafiri, kesi zao huahirishwa mara kwa mara hivyo kusababisha mahabusu kutumikia vifungo vyao kabla ya hukumu. Mfano halisi mtuhumiwa anakaa mahabusu miaka minne kabla ya hukumu, hivyo Serikali inaingia hasara ya kulisha mahabusu. Pia kupunguza nguvu kazi ya Taifa kwa kuwaweka gerezani. Nashauri Serikali iongeze fedha kwa mahakama ili kuongeza utendaji.