Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Katiba na Sheria

Hon. Mgeni Jadi Kadika

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Katiba na Sheria

MHE. MGENI JADI KADIKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza namshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunipa afya njema na kuniwezesha kuchangia hotuba hii.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ukiukwaji wa haki za binadamu, kwanza kuna jambo la kusikitisha kuhusu vijana wanaokwenda kufanya kazi za ndani katika nchi ya Uarabuni- Dubai. Vijana hawa wanateswa, wananajisiwa, wanauliwa lakini hawana watetezi. Je, ni kwa nini Balozi zetu wanakaa kimya na kwa nini hawafuatilii matokeo haya? Huu ni ukiukwaji wa haki za kibinadamu kwa hiyo Serikali yetu ya Tanzania ifuatilie tatizo hili ni kubwa, Watanzania wetu wanapotea.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu Masheikh wetu wa upande wa Zanzibar walishikwa huku Bara sasa ni miaka minne wako mahabusu mpaka leo upelelezi haujapatikana, basi sasa waachiliwe huru wakaishi na familia zao kwa sababu jambo hili linaonekana ni la kisiasa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu Mahakama ya Kadhi, Mahakama ya Kadhi ni chombo cha Kisheria kwa dini ya Kiislam. Chombo hiki ndicho kinachosimamia mirathi na ndoa. Ni kwa nini nchi hii ina Waislamu wengi na inazuia chombo hiki?
Mheshimiwa Mwenyekiti, nchi nyingi duniani zinazo Mahakama ya Kadhi kama vile Kenya, Uganda, Zanzibar na kadhalika. Je, ni lini chombo hiki kitafanya kazi hapa Tanzania bara kwa faida ya Waislam wa nchi hii? Naomba Waziri atakapofanya majumuisho nipate ufafanuzi tafadhali.
Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya mchango huu, naomba kuwasilisha.