Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Katiba na Sheria

Hon. Mbaraka Kitwana Dau

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Katiba na Sheria

MHE. MBARAKA K. DAU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze kwa kumpongeza Mheshimiwa Waziri wa Sheria na Katiba Palamagamba Kabudi. Nianze na hali za Mahakama zetu nchini hususan Mahakama za Mwanzo. Hali za majengo, watumishi na vitendea kazi ni mbaya sana. Katika Wilaya ya Mafia tuna Mahakama ya Mwanzo moja tu na imechakaa na haina watumishi wa kutosha. Wananchi wa Mafia wanalazimika kusafiri masafa marefu kwenda kufuata huduma za Mahakama.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nichukue fursa hii kuiomba Serikali ituongezee Mahakama za Mwanzo angalau mbili katika maeneo ya Utende na Vunjanazi sambamba na kuimarisha vitendea kazi na kuongeza watumishi wa Mahakama ya Wilaya.
Mheshimiwa Mwenyekiti, haki ya dhamana kuu mahabusu kwenye rumande zetu kuna mahabusu wengi wanashikiliwa katika mahabusu zetu wakati wapo wenye kukidhi vigezo vya kumchukulia dhamana. Namwomba Mheshimiwa Waziri wakati wa kuhitimisha hoja alitolee ufafanuzi hili jambo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, upo umuhimu wa Serikali kuongeza bajeti ya Wizara hii ili kuhakikisha suala la utoaji wa haki nchini linafanyika kwa weledi wa hali ya juu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana na naomba kuunga mkono hoja.