Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mpango wa Pili wa Maendeleo wa Taifa kwa kipindi cha Miaka Mitano kuanzia mwaka 2016/2017 – 2020/2021

Hon. Charles John Mwijage

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muleba Kaskazini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Mpango wa Pili wa Maendeleo wa Taifa kwa kipindi cha Miaka Mitano kuanzia mwaka 2016/2017 – 2020/2021

WAZIRI WA VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ninakushukuru kwa kunipa fursa ya kuchangia Hotuba ya Waziri wa Fedha na Mipango kuhusu Mpango wa Pili wa miaka mitano.
Mheshimiwa Naibu Spika, dhima ya Mpango wa Pili wa miaka mitano ni kujenga uchumi wa viwanda ili kuchochea mageuzi ya kiuchumi na maendeleo ya watu. Ninaunga mkono dhima hiyo, nikijibu michango ya Waheshimiwa Wabunge, nataka niwaeleze, ukisoma falfasa ya viwanda, watalaam wa falsafa ya viwanda wanakwambia kujenga uchumi wa viwanda ni vita na ukirejea maandiko ya Mwalimu, mnapokwenda vitani lazima wote muungane mkono. Kwa hiyo, Waheshimiwa Wabunge kwa niaba ya Watanzania niwaombe tuunge mkono ujenzi wa uchumi wa viwanda, asitokee mtu akabaki nyuma.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa nini ni vizuri kujenga uchumi wa viwanda? Uchumi wa viwanda unatusaidia kutengeneza ajira. Watanzania wenzangu mkubali, Tanzania ni Taifa changa kama Afrika lilivyo continent changa, zaidi ya asilimia 65 ya Vijana wetu au watu wetu wana umri wa usiyozidi miaka 35, maana yake ni kwamba hawa watu wanataka ajira. Sekta inayoweza kutengeneza ajira ni viwanda.
Mheshimiwa Naibu Spika, sasa tunakwenda kwenye kitendawili cha viwanda gani tunavitengeneza! Kama alivyosema pacha wangu akirejea usemi wa babu, ukitaka mali utaipata shambani. Tutalenga sekta ambazo zitawashirikisha watu walio wengi na watu walio wengi wapo katika sekta zile za kilimo.
Mheshimiwa Naibu Spika, hivyo niwashawishi Watanzania, sisi mali tunazo, viwanda vitakavyotutoa ni viwanda ni viwanda vidogo sana, viwanda vidogo na viwanda vya kati, hivi ndivyo viwanda vitakavyotutoa, niwahakikishie Watanzania wanao uwezo wa kufanya hivyo. Badala ya kujenga nyumba ukifanya tathmini ya nyumba zilizojengwa katika Miji, zile zinazoitwa dead capital, dead capital unajenga nyumba yako ya ghorofa unafika ghorofa ya tatu huwezi kuendelea, hiyo inaitwa dead capital, ukiorodhesha nyumba zote ambazo ni dead capital au zile zinazojengwa zikaisha zikawekwa vibao vya tunapangisha kwa miaka sita hizo zote ukijulisha na uka-convert pesa yake ukaiweka kwenye viwanda vidogo na viwanda vya kati, vijana wote watapata ajira.
Mheshimiwa Naibu Spika, nitumie fursa hii kuwapa utangulizi wa kazi ambayo nitaifanya kwa miaka mitano ni kuwahimiza Watanzania tubadilishe sasa mtazamo ili tuwekeze kwenye viwanda. Jambo la kuwaambia Watanzania ni kwamba sera ipo, Sustainable Industry Development Policy ipo ya mwaka 1999 mpaka inakwenda mpaka 2020, tunao mkakati unaitwa Integrated Industrial Development Strategy ipo ya 2025.Waheshimiwa Wabunge niwadokeze kitu kimoja kuhusu suala la Kurasini, suala la Kurasini linapotoshwa!
Mheshimiwa Naibu Spika, niwape siri ya Kurasini Logistic Industrial Area tunalenga kwamba sisi tuwe kituo cha mauzo ya nchi zilizotuzunguka, huwezi kuzuia China kuuza nchi za Afrika. China ni soko kubwa sasa tunawaleta hapa. Pia niwape siri msiwambie watu, tunalenga kudhibiti bidhaa substandard tunataka bidhaa zote zitengenezwe Kurasini, bidhaa ambazo ni substandard hazitaingia hapo, ndiyo mpango mzima na wanaotetea wanaogopa hiyo! Hakuna substandard itaingia pale itaanzishwa kitu kinaitwa Total Quality Management (TQM), TBS ambayo iko chini yangu nitawahamishia pale kila kitu kinachoka China kitengenezwe pale na msiwe na wasiwasi kwamba Kurasini itaharibu viwanda.
Mheshimiwa Naibu Spika, leo nina orodha ya wawekezaji, kuna mwekezaji mmoja anakwenda Tanga anatengeneza kiwanda cha saruji tani milioni 2.5 huyu anazuiliwa na Kurasini? Kuna mtengenezaji wa vigae nimempeleka Mkuranga, muulize Mbunge wa Mkuranga atatengeneza square kilometer 80,000 ambazo zitatosheleza Afrika yote, huyu anazuiliwa na Kurasini? kama walivyosema uulize jambo uelezwe, kwa hiyo, kila kitu kina mpango wake.
Mheshimiwa Naibu Spika, nizungumzie EPZ. EPZ ni muhimu na inatenguwa kile kitendawili cha wepesi wa kufanya shughuli. Wawekezaji hasa vijana wanaotoka shule wameshindwa kufanyakazi kwa sababu hawakupa maeneo ya kufanyia kazi. Maelekezo ya Serikali ni kwamba kwenye Halmashauri za Miji kuanzia Vijiji, Kata, Tarafa mtenge maeneo mkija ngazi ya Kanda inakuwa ni EPZ na wale wanaodai tunapambana kuhakikisha wote wanalipwa. Hii ina maana kwamba tukitengeza EPZ tukatengeza maeneo, wawekezaji wanaokuja kuwekeza, Watanzania tunawapa maeneo wanaanza shughuli, na wale wanaotoka nje tutawaelekeza kwenye EPZ.
Mheshimiwa Naibu Spika, ngoja niwape taarifa muelewe. Viwanda vya dunia vilivyokuwa Asia sasa vinarudi Afrika. Viwanda vya dunia nzima vilivyokuwa vimekwenda Asia vinakuja Afrika na mtu asikudanganye, Afrika maana yake ni Tanzania! Kwa hiyo, EPZ zimeandaliwa kuwapokea. Ninazo square kilometers 100 ziko Bagamoyo, Songea nitawafidia, napeleka kwetu Kigoma, iko ile ya Manyoni, nakwenda Bunda - Mara kuweka EPZ na wanaodai wote watapewa fidia. Watu wa Tabora wamelalamikia EPZ, EPZ pitieni ngazi ya Mkoa malizeni matatizo yenu, niiteni mimi ndiyo mwenye mamlaka ya EPZ nitawapa.
Mheshimiwa Naibu Spika, watu wa Dodoma wameniuliza pale nje kwamba Dodoma mbona hamna EPZ, Mbunge wa Dodoma usiwe wasiwasi EPZ nitawapa. Mimi ndiyo mwenye mamlaka ya kutoa EPZ. Tengenezeni mazingira, wakaribisheni Wawekaezaji lazima tutengeneze uchumi wa viwanda.
Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru naunga mkono hoja.