Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Katiba na Sheria

Hon. George Malima Lubeleje

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpwapwa

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Katiba na Sheria

MHE. GEORGE M. LUBELEJE: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza napenda kukupongeza kwa hotuba yako nzuri. Pia naunga mkono kwa asilimia mia moja pamoja na kuunga mkono hoja hii naomba kuchangia maeneo yafuatayo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, upungufu wa Mahakimu wa Mahakama za Mwanzo. Mahakimu wa Mahakama ya Mwanzo ni wachache sana hapa nchini. Wilaya yangu ya Mpwapwa ina Kata 33 lakini PCM wapo wanne tu na hawana usafiri, angalau PCM wote nchini wangepata pikipiki au magari madogo ya kuwasaidia kutembelea Mahakama za mbali kuliko ilivyo sasa PCM wengi wanapanda mabasi ambapo ni hatari hasa PCM akiwa na mafaili ya kesi anaweza kuporwa ndani ya basi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia Mahakimu wa Mahakama za Mwanzo wajengewe nyumba za kuishi badala ya kuishi mitaani ambapo ni hatari kwa maisha yao, bahati mbaya anaweza kupanga na mtu mwenye kesi katika Mahakama yake. Maslahi ya PCM ni duni sana waongezwe mishahara ili kumudu mazingira wanayoishi au kuboresha maisha yao kuliko hali ilivyo sasa. Wilaya ya Mpwapwa tulijengewa jengo la Mahakama ya Wilaya lakini Rest House ya Mheshimiwa Jaji haikujengwa mpaka sasa. Je, itajengwa lini?
Mheshimiwa Mwenyekiti, nashauri kila Tarafa zijengwe Mahakama za Mwanzo nne ili kuwasogezea wananchi huduma ya Mahakama karibu kuliko hali ilivyo sasa wananchi hutembea kilomita zaidi ya 100 kufuata huduma hiyo. Chuo cha Mahakama Lushoto waongeze wanafunzi ili kuongeza idadi ya PCM hapa nchini.