Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Katiba na Sheria

Hon. Kasuku Samson Bilago

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Buyungu

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Katiba na Sheria

MHE. KASUKU S. BILAGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ukosefu wa Mahakama ya Wilaya ya Kakonko; Wilaya ni mpya ina Mahakama za Mwanzo tatu, ambazo hata moja hakuna hakimu (aliyekuwepo yuko masomoni) kama Wilaya tuna kiwanja cha kujenga Mahakama ya Wilaya. Ombi naomba kujengewa Mahakama; na mbili naomba Mahakama ya Mwanzo Kakonko ipewe Hakimu ili kupunguza umbali kwa wananchi kufuata huduma hiyo wilaya jirani ya Kibondo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, wananchi wa Burundi kukamatwa ovyo na kufungwa bila kosa lolote. Polisi wanakuwa wakiwakamata warundi wanaokuja kufanya biashara Kokonko (Jimbo la Buyungu) kwa kukutwa sokoni kuwa ni wahamiaji haramu. Matokeo yake hata wanaokuja kulima vijiji vya jirani Burundi na kurudi jioni kwao nao hukamatwa na kufungwa vifungo bila kujadili ni nchi ya Afrika Mashariki. Wapo warundi wapatao 254 wamefungwa gereza la Nyamisinyi- Kibondo kwa makosa kama hayo. Kimsingi Burundi na raia wake pamoja na sisi tunaopakana nao hatufaidi kuwa kwenye Jumuiya ya Afrika Mashariki.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mapendekezo, Warundi waruhusiwe kuja Wilayani Kakonko kulima na kurudi kwao (uwekwe utaratibu). Warundi wanaokuja kufanya biashara wasikamatwe na kufungwa. Sheria ya kukamata ovyo iangaliwe upya.
Mheshimiwa Mwenyekiti, polisi kubambikiza kesi wananchi, kesi nyingi ni za kubambikiza tu na hivyo kujaza wafungwa gerezani wasio na hatia. Polisi Kakonko wamekuwa wakiwabambikiza kesi wananchi, sheria zilizopitwa na wakati zifanyiwe marekebisho hapo Bungeni. Mfano Sheria ya Ndoa ya 1971.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mashauri kuchelewa kupelekwa mahakamani. Kumekuwa na tatizo la mashauri kutopelekwa Mahakamani mapema hivyo kuwekwa polisi zaidi ya saa 24.