Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Katiba na Sheria

Hon. Dr. Haji Hussein Mponda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Malinyi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Katiba na Sheria

MHE. DKT. HAJI H. MPONDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naanza kwa kuunga mkono Hoja. Wilaya ya Malinyi ni miongoni mwa wilaya mpya na zilizoko katika mazingira magumu (pembezoni). Hivyo, wahitaji kupewa kipaumbele na jicho la kipekee. Wilaya ya Malinyi haina Mahakama ya Wilaya hivyo, hutegemea Wilaya jirani (mama) Ulanga. Tumepeleka maombi ya kuanzisha au kujengewa majengo ya Mahakama ya Wilaya ya Malinyi. Tunaomba Serikali kulipa kipaumbele ombi hili la ujenzi wa Mahakama ya Wilaya kwa kuwa huduma hiyo inapatikana mbali sana kilomita 200 hadi 300 toka Wilayani Malinyi kwenda Ulanga.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Wilaya ya Malinyi ina Mahakama za Mwanzo mbili tu kuhudumia wilaya nzima yenye ukubwa wa kilomita za mraba 10,576 na idadi ya watu karibu 250,000. Hivyo tunaomba tuongezewe Mahakama za Mwanzo. Aidha, Mahakimu waliopo wa Mahakama za Mwanzo wamekuwepo muda mrefu katika vituo vyao vya kazi; hivyo kuathiri sana utendaji/ufanisi wa majukumu yao ya kazi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba Wizara iweke na kumwezesha Hakimu wa Wilaya ya Ulanga ambaye pia anahudumia Wilaya ya Malinyi kuja kusikiliza mashtaka (kesi) katika Wilaya ya Malinyi ili kuepusha au kupunguza usumbufu kwa watuhumiwa kwani wanapata adha kubwa sana kwenda na kurudi Mahenge (Ulanga). Ahsante.