Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira

Hon. Prof. Sospeter Mwijarubi Muhongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Musoma Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira

WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kutoa tu ufafanuzi kwa mambo mawili yaliyoongelewa. Kwanza ni deni la umeme la Zanzibar; napenda kuwaeleza Waheshimiwa Wabunge kwamba tunayo Kamati ambayo inaongozwa na Makatibu Wakuu wa pande zote mbili na wiki ijayo watakuja na nyaraka. Kuna maeneo wamekubaliana kuna maeneo hawakukubaliana. Kwa hiyo, nitaitisha kikao na mwenzangu wa Zanzibar ili jambo la deni la umeme tutalimaliza. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nije kwenye suala la mafuta na gesi. Kwanza siyo limetolewa kwenye mambo ya Muungano, mimi mwenyewe nilikaribishwa kwenda Zanzibar wakati ambapo Sheria ya Zanzibar ya mwaka 2016 inazinduliwa na Mheshimiwa Rais wa Zanzibar. Ambacho ni
muhimu na nimekisema mara nyingi, tusipende kuongea mafuta, mafuta, gesi, gesi nadhani cha kwanza kabisa tujue je, hayo mafuta yapo? Hiyo gesi ipo?
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, kitu cha kuongelea hapa kwanza tujue kwamba kweli yapo au hayapo, hilo la kwanza. La pili, kama yapo, hiki kugawana siyo kitu ambacho ni kigeni duniani hapa. Sisi Tanzania tumeanza majadiliano kwa gesi au mafuta yaliyoko Ziwa Tanganyika lazima tukae chini na Kongo, Zambia na Burundi, hatuwezi kukwepa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, huku chini Msumbiji ni lazima tufanye majadiliano na wenzetu wa Msumbiji tukienda kwenye vitalu vya kusini kabisa. Hiki siyo kitu kigeni duniani kinafahamika, kuna sheria za Kimataifa, kwenye Arctic Circle kuna mafuta mengi sana kule na gesi, inabidi Urusi na Ulaya wajadiliane. Kwenye mipaka ya Marekani na Canada kuna gesi na mafuta na wenyewe wanajadiliana. Nigeria na Cameroon wanajadiliana. Hivyo, ni vizuri exploration ifanyike upande wa Zanzibar tujue mafuta yako wapi au gesi iko wapi tukishapata ile ndiyo tutajadili namna ya kushirikiana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kama yako upande wa Zanzibar ni mafuta yao, kama yako upande wa Bara ni mafuta yao, lakini kama yako katikati hayakuheshimu mipaka ya kisiasa na ambavyo mara nyingi ndivyo inavyotokea, kwa sababu hivi ni vitu vilivyotengenezwa kati ya miaka milioni 55,200, Zanzibar haikuwepo, Bara haikuwepo hata Indian Ocean ndiyo ilikuwa inaanza kutengenezeka. Kwa hiyo, tuna taratibu za Kimataifa za namna ya kushirikiana kwenye rasilimali kama hiyo. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa upande wa Zanzibar labda wanasiasa watalumbana sana lakini upande wa wataalam sisi tulitoa ahadi kuwasaidia wenzetu wa Zanzibar. Hata wiki jana badala ya kupeleka vijana Watanzania Bara 20 kwenda kusoma China mambo ya mafuta na gesi, kwa
kuwa nilitoa ahadi kwa Serikali ya Zanzibar nafasi tano tumepatia wenzetu wa Zanzibar waende kusoma kule China. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, niwatoe hofu watu wanaosema mafuta kwanza, yakipatikana Magharibi mwa Pemba nachukulia mfano, huenda tusikwepe kujadiliana na Kenya. Kwa sababu ukiangalia mpaka wetu ukiuchora unavyokwenda huko juu kabisa ya Pemba, Pemba iko hapa, mpaka unapita hapa. Sasa kama mafuta yanaingia Kenya tutafanyaje? itabidi tujadiliane Zanzibar, Bara na Kenya. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, hili jambo kitaalam ni la kawaida, wala msisumbuke ninyi tulieni. Ahsante.