Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira

Hon. Richard Mganga Ndassa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sumve

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira

MHE. RICHARD M. NDASSA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono na nawapongeza sana hasa kwa kuamua kulisimamia suala la upandaji na utunzaji wa miti. Kwimba tulipata ugeni wa Makamu wa Rais ambapo tulimweleza mipango yetu ya kupanda na kuitunza ambapo tunaanzia kwenye shule za msingi na sekondari. Tumekubaliana kila mwanafunzi anayeanza shule awe na mti wake ambao utapewa jina lake ambapo atautunza hadi amalize darasa la saba.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hivyo, mwanafunzi huyo huyo akiingia darasa la pili, tatu, nne, tano, sita na saba kila darasa atakuwa na mti wake, kwa hiyo akimaliza darasa la saba mwanafunzi mmoja atakuwa na miti saba. Mfano
Shule ya Msingi Kadashi ina wanafunzi 1000, kwa utaratibu huo kutakuwa na upandaji na utunzaji wa miti 1000, hii ni kwenye eneo moja la Shule ya Msingi Kadashi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Shule ya Sekondari ya Wasichana ya Askofu Mayala aliyotembelea Makamu wa Rais, Mheshimiwa Samia Suluhu, kuna wanafunzi zaidi ya 200, hivyo kila mwanafunzi anapoanza kidato cha kwanza hadi cha nne akimaliza form four atakuwa ameacha miti iliyopandwa na kutunzwa miti 800 ikiwa na majina yao. Upandaji wa miti na utunzaji wa miti kwa ajili ya mbao, kivuli, matunda na utunzaji mazingira. Naomba Wizara yako endapo kuna fungu lolote Kwimba iwe pilot area katika suala zima la upandaji na utunzaji wa miti. Kauli mbiu yetu ni ‘upandaji na utunzaji wa miti kwa manufaa ya vizazi vilivyopo na vijavyo’.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tuwe kama vichaa katika kupanda na kutunza miti.