Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mpango wa Pili wa Maendeleo wa Taifa kwa kipindi cha Miaka Mitano kuanzia mwaka 2016/2017 – 2020/2021

Hon. Mahmoud Hassan Mgimwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Mpango wa Pili wa Maendeleo wa Taifa kwa kipindi cha Miaka Mitano kuanzia mwaka 2016/2017 – 2020/2021

MHE. MAHMOUD H. MGIMWA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nichukue fursa hii kumpongeza sana Mheshimiwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli kwa kazi nzuri anazozifanya. Naomba nimpongeze Dkt. Mpango kwa uwasilishaji wake mzuri.
Naomba kuishauri Serikali katika mambo yafuatayo:-
Ni vyema kuweka wazi mafanikio na changamoto zilizojitokeza katika Mpango wa Kwanza 2011 – 2016 ili tujue tatizo ni nini? Serikali imeamua maamuzi yapi kwa yale mambo ambayo bado hayajakamilika.
Mpango huo ulilenga kutanzua vikwazo vya kiuchumi na kupunguza umaskini na kuimarisha upatikanaji wa huduma za jamii.
Mheshimiwa Naibu Spika, ukuuaji wa pato la Taifa 6.7% - 7% unalingana na upatikanaji wa huduma za jamii kama afya, maji na elimu.
Mheshimiwa Naibu Spika, ukuaji wa uchumi uende sambamba na kupunguza umaskini.
Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Waziri alipaswa kuweka wazi vigezo vilivyotumika kujua uchumi wa Taifa unakua, income per capita peke yake hatoshi kwa sababu upatikanaji wa income per capita unajumuisha matajiri sana na maskini sana.
Mheshimiwa Naibu Spika, mfumuko wa bei unasababishwa mara nyingi na cost push inflation na demand pull inflation. Naipongeza sana Serikali kwenye eneo la demand pull inflation ni muda mrefu sasa tumeweza kuhimili mahitaji ya chakula ndani ya nchi lakini kwenye cost push inflation.
Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Waziri ametaja eneo la mafuta, ni vyema Serikali ikajipanga kuhakikisha umeme wa uhakika unapatikana na wa bei nafuu. Serikali ihakikishe umeme wa makaa ya mawe, maji na upepo unapatikana ili kupunguza adha ya umeme.
Mheshimiwa Naibu Spika, pia Serikali ihakikishe barabara za uhakika maeneo yote yenye kilimo cha uhakika kwa lengo la kupunguza gharama pia reli ianze kufanya kazi kwenye maeneo yote muhimu.
Mheshimwa Spika, eneo lingine ni kuhusu thamani ya shilingi ambayo inashuka na haiko stable.
Mheshimiwa Naibu Spika, ni vyema sasa Serikali ikaweka mkakati wa kuondoa matumizi ya dollarization ambayo nchi nyingi duniani zimedhibiti eneo hili.
Mheshimiwa Naibu Spika, tunauza kidogo nje ya nchi kuliko tunavyonunua. Ni vyema sasa tujidhatiti kuongeza kuuza nje ya nchi.
Mheshimiwa Naibu Spika, kilimo; asilimia sabini na tisa ya Watanzania inategemea kilimo, ni vyema tukajipanga katika eneo hili.
Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja.