Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira

Hon. Daniel Nicodemus Nsanzugwako

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kasulu Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira

MHE. DANIEL N. NSANZUGWANKO: Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja hii. Hata hivyo nina machache ya kuchangia.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hoja ya uharibifu mkubwa wa mazingira ulisababishwa na ujio wa maelefu ya wakimbizi toka Burundi, DRC na Rwanda. Ujio huu umesababisha uharibifu mkubwa wa mazingira katika Wilaya ya Kasulu, Kibondo na Kakonko, idadi ya wakimbizi sasa ni zaidi ya 600,000. Ajabu ni kwamba katika hotuba yote ya Waziri hakuna hata mistari wala aya inayoelezea uharibifu huo wakati madhara yake kwa wakazi wa Mkoa wa Kigoma ni makubwa sana. Naishauri Serikali/Wizara ije na mpango maalum wa kuhifadhi mazingira na au kufufua maeneo yaliyoharibika sana na ujio wa wakimbizi. Mfano:
(i) Mto Makere umekufa na kukauka kabisa
(ii) Misitu katika vijiji imekatwa sana na kuharibiwa kabisa
(iii) Vyanzo vya maji (water resources) nyingi zimeharibika kabisa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, “we need comprehensive program to restore the environment on area hosting refugees and communities hosting refugees in Kigoma”
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mkakati wa kuhifadhi vyanzo vya maji katika Wilaya ya Kasulu na hasa vyanzo vilivyopo Kasulu Mjini. Katika eneo la Kasulu Mjini tuna vyanzo zaidi ya
200. Naomba jitihada za pamoja za Serikali/Wizara na Halmashauri ya Mji kulinda vyanzo vya maji ambavyo hatimaye hupeleka/hutiririsha maji yake katika Ziwa Tanganyika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana hatua ya Waziri kutuma wataalam wa Maji na Mazingira kuja Wilaya ya Kasulu kufanya “study Project on that one”. Hatua ni njema.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mfuko wa Taifa wa Mazingira; nashauri tozo zinazotozwa na TFS na migodi iliyopo nchini angalau asilimia 25% ya tozo hizo zipelekwe kwenye Mfuko huo ili kulinda Mazingira ya Taifa letu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mfano mwaka 2015/206 – TFS walikusanya zaidi ya shiligi billioni 50 ingekuwa busara sana kama 25% ya fedha hizi zingepelekwa kwenye mfuko huo. Tozo toka mgodini ni fedha nyingi sana na kwa hali ilivyo sasa hakuna hata senti inayopelekwa kwenye mazingira.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara inaweza kuleta pendekezo la sheria Bungeni ili sheria hiyo tuitunge haraka sana kwa mwaka wa fedha 2017/2018.