Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira

Hon. Mbaraka Kitwana Dau

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira

MHE. MBARAKA K. DAU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze kwa kutoa pongeza nyingi kwa Mheshimiwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Muungano na Mazingira, Mheshimiwa January Yusuf Makamba na Naibu wake Mheshimiwa Luhaga Mpina
Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze kwa kuelezea ari kubwa ya kimazingira inayokikabili Kisiwa cha Mafia na visiwa vidogo vidogo vinavyoizunguka Mafia. Mabadiliko ya tabia nchi kwa kiasi kikubwa vinatishia kuviondoa kabisa kwenye uso wa dunia visiwa vya Bwejuu, Jibondo, Chole na Juani.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ongezeko la kina cha bahari limepelekea kiasi kikubwa cha ardhi ya visiwa hivyo kumeguka. Kwa Muktadhi huu natarajia Mheshimiwa Waziri wakati wa kuhitimisha hoja yake aje atueleze wananchi wa Mafia hatua ambazo Serikali inachukua katika kuokoa visiwa hivi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mafia ni Kisiwa chenye vyanzo vichache vya maji lakini kutokana na kukua kwa shughuli za kijamii vyanzo hivi vimeanza kuvamiwa na mvuto hali hii inatishia upatikanaji wa maji safi na salama, nichukue fursa hii kwa namna ya kipekee kumwomba Mheshimiwa Waziri au Naibu wake kuja kutembelea Mafia ili kujionea hali ilivyo kimazingira .
Mheshimiwa Mwenyekiti, uchafu unaotupwa katika Bahari yetu ya Hindi kwa kiasi unatokana na mifuko ya Plastic (maarufu kama mifuko ya rambo). Kwa namna ya kipekee kabisa napenda kuomba Serikali yangu Tukufu kupiga marufuku matumizi ya mfuko na vifungashio vya plastic
Mheshimiwa Mwenyekiti, niliwahi kusoma Jarida moja la uchunguzi la Kimataifa, likitoa Matokeo ya Uchunguzi ya kuonyesha kuwa kama hali ya utupaji taka baharini ilivyo sasa ikiendelea vivi hivi ifikapo mwaka 2050 ndani ya bahari kutakuwa na takataka nyingi (hususan) mifuko ya plastic kuliko idadi ya samaki. Hivyo, ipo haja sasa ya kupiga marufuku mifuko ya plastic.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ukataji miti kwa madhumuni ya kuchoma mkaa, sasa ni janga la Kitaifa. Naipongeza Serikali kwa hatua mbalimbali ilizochukua kupiga marufuku uchomaji na usafirishaji wa mkaa. Niiombe Serikali kupunguza bei ya gesi ili wananchi wengi waweze kuhama kwenye kutumia mkaa na kutumia gesi asilia.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kumalizia niwatakie Watanzania wote kwa kusherehekea Muungano wa Tanganyika na Zanzibar.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.
Ahsante sana.