Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira

Hon. Richard Phillip Mbogo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nsimbo

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira

MHE. RICHARD P. MBOGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza natoa pongezi kwa Waziri na timu yake kwa hotuba nzuri ya bajeti.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mazingira ni Mtambuka, suala la mazingira ni muhimu sana katika utunzaji na faida zake, vilevile umuhimu katika maisha ya wanadamu. Wizara takribani nne zinaingiliana katika utunzaji na usimamizi wa mazingira; TAMISEMI, Maliasili na Utalii, Ardhi, Maji na Mazingira. Hivyo basi, usimamizi katika maeneo mengi umekuwa hafifu kutokana na fedha, rasilimali watu, vitendea kazi pia Wizara kukosa wawakilishi katika maeneo mengi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hivyo basi, naiomba Serikali ifanye mpango ambao utakuwa unaweka mawasiliano mazuri ambayo yatakuwa na tija. Mfano, mabonde ya maziwa mbalimbali hayana usimamizi wa moja kwa moja kwenye vyanzo vyote vya mabonde kwa kuwa ofisi za mabonde zipo Kikanda na Halmashauri nyingi hazisimamii mabonde hayo. Tunahitaji Wizara zote hizi kuwa na uhusiano wenye tija.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Upandaji Miti, katika Halmashauri zetu zimeweza kutii maagizo ya kutenga fedha kwa ajili ya upandaji miti, tatizo ambalo litakuwa mbele yetu ni upatikanaji wa fedha za kutekeleza bajeti hiyo, vilevile usimamizi wa kuhakikisha miti inakuwa mfano mzuri, ni wakulima wa Tumbaku ambao upatiwa fedha ili kupewa miti, wengi wao huwa hawatilii maanani kuhakikisha miti inapandwa na kukua.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ruzuku katika nishati, ili kuendelea kulinda mazingira ni muhimu kwa Serikali kuweka ruzuku katika nishati mbadala ambazo zitakuwa zinalinda mazingira, mfano matumizi ya gesi, nishati ya jua kuokoa au kupunguza matumizi ya mkaa ambao unapelekea ukataji mkubwa wa miti.