Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira

Hon. Selemani Moshi Kakoso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpanda Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira

MHE. MOSHI J. KAKOSO: Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote nawapongeza sana Mheshimiwa Makamu wa Rais na Waziri Makamba kwa juhudi kubwa wanayoifanya hasa katika ziara zinazofanyika katika nchi yetu wakihamasisha suala la hifadhi ya mazingira.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimpongeze Waziri alipokuja Mpanda na kutoa amri ya kuondoa mabanio ya Mto Katuma ambao ulikuwa unakaribia kutoweka. Ombi langu tunaomba Ofisi yako itoe fedha kwa ajili ya kuwasaidia wananchi wanaotunza Mto wa Katuma wasaidiwe fedha za kuchimba mabwawa na malambo yatakayosaidia kuacha uharibifu wa mto huo ambao ni muhimu kwa ajili ya Hifadhi ya Katavi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, eneo lingine ni hifadhi za misitu, ni vema suala la kuhifadhi misitu iliyopo Mpanda wasiachiwe watu wa maliasili pekee kwani suala hili ni muhimu sana katika kuhifadhi misitu ambayo inafyekwa kwa shughuli za kilimo, ufugaji na nishati ya kuni. Niiombe Serikali iangalie suala hili kwa uzito mkubwa kwani shughuli hizi za binadamu zinatumia sana misitu na kutengeneza uharibifu wa mazingira. Ushauri wangu ni;
(i) Serikali isimamie suala la kilimo cha kuhamahama;
(ii) Wafugaji wafuge ufugaji wa kisasa ili tupunguze wingi wa mifugo; na
(iii) Serikali iandae mpango wa kuwawezesha Watanzania wapate gesi kwa bei nafuu ili waachane na suala la kutegemea kuni.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Hifadhi ya Ziwa Tanganyika na Ziwa Rukwa; Ziwa Tanganyika linaendelea kupungua siku hadi siku. Kama Serikali haitachukua hatua stahiki ziwa hili litapungua sana siku hadi siku. Serikali ichukue hatua ya kuweka banio nchini DRC Kongo, bila kufanya hivyo Ziwa Tanganyika litatoweka.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Ziwa Tanganyika limejaa tope, Wizara nendeni na mpeleke wataalam waangalie uwezekano wa kutoa tope na kulifanya Ziwa hilo liwe hai.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.