Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira

Hon. Elias John Kwandikwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira

MHE. ELIAS J. KWANDIKWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naanza kwa kuunga mkono hoja. Napenda kutoa mchango wangu kwa kuishauri Wizara hii kusimamia fedha wanazochangia wananchi wakulima wa tumbaku kupitia tozo kwenye mauzo yao namna zinavyotumika kwenye kuhifadhi Mazingira.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Waheshimiwa wabunge wajue tozo ni kiasi gani zimekusanywa na kiasi hicho kimerejeshwa kwenye maeneo yaliyoathirika na uharibifu wa mazingira; kwani kuna uwezekano zikatengenezwa taarifa za fedha zilizotumika ambazo siyo sahihi kwani wananchi binafsi wanajihusisha kuhifadhi mazingira. Isije ikatokea kuwa na utaratibu hafifu fedha za tozo kwenye tumbaku zikatumika na wajanja na wakasingizia zimetumika kwa kubadilisha na juhudi binafsi za wananchi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante na naunga mkono hoja.