Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira

Hon. Sophia Hebron Mwakagenda

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba Ofisi ya Makamu wa Rais ipatiwe bajeti yake yote ili iweze kutimiza kazi zake kiukamilifu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Uchaguzi Zanzibar, Serikali ya Muungano haitaki kuiacha Zanzibar huru ifanye kazi zake kwa matakwa yake bali Tanganyika inaingilia chaguzi na hata maamuzi ya Wazanzibari hapa na pale. Inaendelea kuikandamiza CUF katika utendaji kazi za kisiasa na kero za Zanzibar bado mpaka sasa zinasuasua na sina hakika kama ziko tisa .
Mheshimiwa Mwenyekiti, usalama wa raia toka uchaguzi wa mwaka 2015 Zanzibar haiku shwari kwani ule umoja wa Wazanzibar kwa sasa haupo baada ya kuwa na makundi mawili mahasimu wa kisiasa yaani CCM na CUF.
Mheshimiwa Mwenyekiti, vijana wengi na wananchi waliumizwa katika marudio ya upande mmoja wa CCM na kuweka ari ya sintofahamu kwa raia baada ya Jeshi la Polisi na JKU kutanda mitaani na kutishia raia. Huu si utamaduni wetu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katiba mpya; ni wazi tumepoteza pesa nyingi sana kwa kuanzisha mchakato huu kwani matakwa ya wananchi hasa ilipotokea kuachwa kwa rasimu ya katiba ya Mheshimiwa Warioba ambayo CCM iliacha na kutengeneza rasimu isiyokuwa na matakwa ya wananchi. Naomba tuanzie pale wananchi walipotaka kwenye katiba ya Warioba.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kesi za kusingiziwa; kumekuwa na mashtaka ya kubambikiwa kesi katika Serikali ya Muungano hasa kwa wafuasi wa CUF. Tunaomba Wizara hii ichukue nafasi yake ya upatanishi na kusimamia haki.