Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira

Hon. Issaay Zacharia Paulo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira

MHE. ZACHARIA P. ISSAY: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuishauri Serikali ifuatavyo:-
(i) Serikali itazame upya bei za gesi asilia kwani kwa sasa ni ghali ukilinganisha na maisha ya Mtanzania;
(ii) Serikali ifanye mapitio maeneo yenye makazi ya wananchi kwa wale wanaoishi karibu na vyanzo vya maji na maeneo ya miinuko katika nchi yetu. Mfano; wananchi hao wanaweza kufanya shughuli rafiki wa mazingira;
(iii) Serikali iangalie uwezekano wa kunusuru maeneo yenye uoto wa asili ili kuwa endelevu kwa kizazi kijacho;
(iv) Serikali itoe Waraka kwa DC’s (District Commissioner) na DED’s (District Executive Director) nchini kuhusu upandaji wa miti na mashindano ya Kaya kwa Kaya,
Kijiji kwa Kijiji, Kata kwa Kata na Wilaya kwa Wilaya na mwisho Kitaifa. Siku ya Mazingira ifanyike na kutoa zawadi;
(v) Taasisi mbalimbali ziwe na bustani za miche kama kitovu cha utoaji wa..
(vi) Tunaomba Serikali itusaidie kunusuru Maziwa madogo ya asili katika Mkoa wa Manyara; Ziwa Basutu katika Wilaya ya Hanang; Ziwa Tlawi katika Wilaya ya Mbulu; Ziwa Manyara katika Mkoa wa Arusha Wilaya ya Monduli na Ziwa Babati katika Wilaya ya Babati.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante na naunga mkono hoja kwa asilimia mia moja.