Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira

Hon. Mary Deo Muro

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira

MHE. MARY D. MURO: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuchangia kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, nichangie kuhusu suala zima la uteketezaji misitu na usababishaji wa mabadiliko ya tabianchi ambalo ndiyo tatizo sugu duniani na kwa Tanzania kupelekea kwa sasa mvua kukosekana. Naishauri Serikali kuanzisha njia mbadala ya mkaa tutapunguza ukataji miti, huko nyuma kulikuwa na mpango wa kupunguza ukataji wa mkaa kwa kuanzisha kilimo cha mibono inayotoa moto poa ambayo ingesaidia kuleta chanzo kipya cha moto.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ujenzi na kilimo kwenye vyanzo vya maji; elimu kwa wananchi ni ndogo kuhusu suala hilo. Niishauri Serikali yangu kuongeza juhudi ya kuelimisha wananchi, pia Serikali iangalie uvuvi haramu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ufugaji mifugo mingi na hatari mijini; niishauri Serikali yangu kuhakikisha elimu kwa wafugaji mifugo inatolewa, upunguzaji mifugo ili kupunguza uharibifu wa mazingira kupitia mifugo mingi kuchungwa kwenye maeneo madogo. Mfano halisi ni ng’ombe wanaochungwa katika Mji wa Dodoma ambao ni Mji Mkuu wa nchi. Niishauri Serikali kuhakikisha inatoa elimu ya kutumia vinyesi vya ng’ombe hao kutengeneza gesi ili kupunguza ukataji miti kwa ajii ya Mkaa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Muungano; niishauri Serikali iendelee kuondoa kero za Muungano kadri zinavyozinduliwa. Niishauri Serikali kuhakikisha inajenga dhana za kujitegemea kwa kutenga fedha za ndani za kutosha kuliko kutegemea wafadhili.
Mheshimiwa Mwenyekiti, niishauri Serikali iongeze fedha za bajeti kwa ajili ya kufanikisha utendaji wa Wizara hii ili kuleta afya kwa wananchi kwani haiwezi kufanya kazi zenye ufanisi bila kuwa na bajeti timilifu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.