Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira

Hon. Zubeda Hassan Sakuru

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira

MHE. ZUBEDA H. SAKURU: Mheshimiwa Mwenyekiti, Mkoa wa Ruvuma wanakabiliana na changamoto nyingi katika utunzaji wa mazingira hasa misitu, hivyo kunahitajika jitihada za makusudi ili kukabiliana nazo. Kwa mfano, Wilaya ya Tunduru haipaswi kuwa maskini kutokana na utajiri wa misitu iliyonayo. Hata hivyo, mojawapo ya kero ni pamoja na mifugo kuvamia katika misitu, hivyo kuhatarisha uendelevu wa misitu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, aidha, wilaya hii ina misitu ya Miombo inayokadiriwa kuwa na ukubwa wa eneo la kilomita za mraba 150,000, hivyo ni dhahiri kuwa uendelezaji wa misitu hii inahitaji uzalishaji mkubwa wa wananchi ili kuleta tija.
Mheshimiwa Mwenyekiti, bado ipo haja ya Serikali kuhakikisha kuwa shughuli za kiuchumi hasa uanzishwaji na uendeshaji wa viwanda unafanyika kwa umakini mkubwa.
Je, mpaka sasa ni viwanda vingapi vimepewa adhabu/faini kwa uchafuzi wa mazingira mpaka Machi mwaka huu na je, ni hatua gani madhubuti zinafanyika kuzuia uchafuzi wa mazingira.
Mheshimiwa Mwenyekiti, bado ipo hoja ya kufanya tathimini ya kitaifa juu ya athari za mazingira hasa katika sekta ya uzalishaji wa viwanda na madini. Napenda kujua ni mkakati gani ambao Serikali imeweka ili kukabiliana na uharibifu wa mazingira hasa katika miradi ya madini na kuangalia jinsi ambavyo migodi hiyo inakidhi matakwa ya kisheria juu ya utumiaji na usimamimzi wa mazingira migodini.
Mheshimiwa Mwenyekiti, utiririshaji wa maji taka nje ya mfumo rasmi wa majitaka hasa kipindi cha mvua umeendelea kuhatarisha mazingira hasa afya za watumiaji wa miundombinu katika miji. Ni dhahiri kuwa, pamoja na kuwa na changamoto za kimazingira na miundombinu, pia ipo haja ya kufanya tathmini ya mfumo kwa utiririshaji majitaka na athari zake kwa mazingira ikiwemo binadamu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha.