Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira

Hon. Lucia Ursula Michael Mlowe

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira

MHE. LUCIA M. MLOWE: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa mabadiliko ya tabianchi ambayo yamebadili majira ya mwaka kwa kuyachelewesha au kuyawahisha na madhara yanayotokea kutokana na mabadiliko hayo mara nyingi yanakuwa ni kuharibika kwa miundombinu na pia watu kupoteza maisha.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, naishauri Serikali iwekeze katika sekta za kuzuia na kupambana na mabadiliko ya tabia nchi. Mfano kusimamia sheria za utunzaji wa mazingira kama vile upandaji miti, kuzuia watu wanaokata miti ovyo na wanaochoma ovyo misitu na kusababisha ongezeko la ukaa. Wachukuliwe hatua stahiki.
Mheshimiwa Mwenyekiti, uzalishaji na matumizi ya mifuko ya plastiki. Kwa kuwa vifungashio vya plastiki vinachafua mazingira, basi naishauri Serikali ione utaratibu wa kufanya recycling ili isiathiri mazingira na isiathiri wananchi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nishati mbadala; ili kupunguza au kuondoa kabisa uharibifu wa mazingira kupitia ukataji wa miti kwa ajili ya kuni na mkaa, basi Serikali waje na mkakati wa kutafuta wawekezaji wajenge kiwanda cha kuchakata gesi hapa Tanzania na kuiweka kwenye mitungi na kuisambaza nchi nzima.
Mheshimiwa Mwenyekiti, takataka; Miji yetu inazalisha taka nyingi zikiwemo taka ngumu na taka za maji. Hakuna mfumo rasmi unaotumika ili kuhakikisha taka mbalimbali zinakusanywa ipasavyo. Naishauri Serikali kuweka mfumo rasmi wa kutupa taka hizo. Naomba kuwasilisha.