Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira

Hon. Susan Limbweni Kiwanga

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Mlimba

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira

MHE. SUSAN L. KIWANGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hotuba ya Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni. Bila mazingira nchi hii tunakwenda kuangamiza vizazi vyote katika nchi hii.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nashauri Serikali iongeze fedha za mazingira katika bajeti. Bajeti ya mazingira kila mwaka haieleweki ingawa suala la mazingira ni mtambuka.
Hivyo ni wakati sasa umefika wa kutilia mkazo suala la mazingira ili kuwepo na watumishi na Idara ya Mazingira. Ni ukweli usiopingika kwamba mazingira yanaharibiwa ngazi ya mitaa na vijiji, mijini na vijijini. Hivyo mkiimarisha Idara hiyo kwa kutengewa fedha za kutosha mtanusuru na kulinda mazingira.