Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira

Hon. Lucy Fidelis Owenya

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira

MHE. LUCY F. OWENYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kupata nafasi ya kuchangia. Utunzaji wa mazingira ni muhimu sana katika kuleta maendeleo, kuleta hewa safi, kuongeza mvua na kadhalika. Sisi wote ni mashahidi katika nchi yetu, kumekuwepo na ukame wa kupitiliza kiasi hata mazao hayawezi kulimwa, vyanzo vya maji vinakauka na kadhalika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ushauri, Serikali kwa kupitia kila Kitongoji na Kijiji zile Kamati za Mazingira ziimarishwe, ziwezeshwe kama ilivyokuwa miaka 30 iliyopita. Ilikuwa ni lazima kupanda miti kila shule kuwa na vitalu vya miche, mfano Kilimanjaro ilikuwa hairuhusiwi kulima au kujenga kandokando mwa mto na mifereji iliyokuwa inatiririka maji na mito lakini sasa hivi yote imekauka.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuyeyuka kwa theluji ya mlima Kilimanjaro, miaka ya hivi karibuni Profesa L. Thomson kutoka University ya Ohio kule Marekani walikuja kufanya utafiti ni kwa nini theluji inapungua kwenye mlima Kilimanjaro, walibeba barafu nyingi sana (in tons) kuzipeleka Marekani. Je, Serikali mmefuatilia walibaini ni kwa nini theluji inapungua katika mlima Kilimanjaro?
Mheshimiwa Mwenyekiti, wakati tukisubiri sababu ni vizuri kuhimiza miti kupandwa kwa wingi ili wananchi waweze kupata maji na mvua, kwa sasa hivi Mji wa Moshi ndio wenye joto kubwa kuliko popote hapa nchini na Moshi ipo chini ya Mlima Kilimanjaro hii ni hali ya hatari sana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ukataji wa miti kwa ajili ya mkaa, ni vizuri Wizara hii na Wizara ya Nishati na Madini waangalie ni jinsi gani wanaweza kushusha bei ya gesi ya kupikia ili kila mwananchi aweze kununua gesi ya kupikia. Hii itasaidia kupunguza uharibifu wa mazingira, miti haitakatwa kwa sababu ya mkaa.