Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Hon. George Mcheche Masaju

Sex

Male

Party

Ex-Officio

Constituent

None

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI: Mheshimiwa
Mwenyekiti, kwanza namshukuru Mwenyezi Mungu kunipa fursa na mimi niweze kuchangia hapa. Nakushukuru wewe pia kwa kunipa nafasi hii.

Pia nachukua nafasi hii kumpongeza sana Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa utendaji wake wa ufanisi uliotukuka sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nawapongeza na Mawaziri wawili wanaomsaidia na timu nzima ya ofisi yake na watendaji wote kwa hotuba nzuri ambayo imeonesha mambo ambayo Serikali imeyafanya katika mwaka huu na inayokusudia kuyafanya mwaka ujao wa fedha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hayo, naomba kushauri mambo yafuatayo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye hili suala la utekaji nyara na mambo ya hofu, yanajitokeza sana hapa na sijui ni kwa nini? Naomba kushauri kwamba polisi waendelee kushirikana na watu walio karibu sana na huyu mtu anayedaiwa amepotea. Waisaidie polisi ili tupate ukweli; kwanza familia yake, watu ambao amekuwa akifanya nao kazi kwa karibu, watoe ushirikiano kama ambavyo Bunge wameshauri. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye suala hili hatuwezi kuwa na double standard. Kwa mujibu wa Katiba Ibara ya 26, kila mmoja anawajibika kutii Katiba na sheria ya nchi. Mheshimiwa Mbowe ametusaidia, kwenye hotuba yake amesema hakuna aliye juu ya sheria. Moja, akatueleza tangu huyu mtu anayedaiwa kupotea au kufariki. Alipopotea, ilichukua muda gani kutoa taarifa? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, halafu familia au watu waliokuwa karibu na huyu mtu, kwa mfano, wameshapeleka taarifa kwenye vyombo vya habari kwamba huyu mtu labda amepotea, hebu mtu yeyote aliyopo kwenye public atusaidie, then tu-take action accordingly. Mimi ninavyojua polisi ilivyokuwa inafanya kazi, siku hizi wanafanyaje kazi? Sasa hivi tungekuwa na watu wanaisaidia polisi kwa karibu mno! Sasa this is how we can handle this matter so much successful. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabla hatujaenda huko Scotland Yard, watu waliokuwa wanafanya kazi kwa karibu na familia y ake, watoe taarifa, vyombo vyetu vifanyie kazi kwa karibu mno, hilo ni la kwanza. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili, hili siyo suala la uhuru wa mijadala humu Bungeni. Ibara ile ya 100 uisome ina vifungu viwili vidogo; kifungu cha kwanza na cha pili, hata uhuru wa mijadala, haukuwekwa uhuru wa haki ya kuvunja sheria. Ukisoma Ibara ndogo ya (1) na ya (2), unayo hiyo haki tu kama katika mjadala wa kutekeleza majukumu yako ya Kibunge unazingatia Katiba na Sheria za nchi, la sivyo, basi wewe ungekuwa tu unaua mtu, unapiga mtu, unasema mimi nina haki sijui ya nini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kushauri tusitumie vibaya uhuru wa mijadala. Hata huku kutangazwa, wanaita matangazo mubashara, someni Ibara ya 100 kama ipo hiyo haki. Someni Sheria ya Haki, Kinga na Mamlaka za Bunge kama ipo hiyo haki ya kutangaza mubashara. Someni Kanuni 143, haki tuliyonayo ni ya Taarifa za Bunge. Ibara ya 18 ya Katiba inatoa haki ya watu kupewa taarifa na mpaka sasa hivi Serikali haijakataza vyombo vya habari kuripoti mambo yanayoendelea humu ndani. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ngoja niwashauri Waheshimiwa Wabunge, kama mnataka kurudi katika Bunge hili, tetedni mambo yanayowanufaisha wapigakura wenu. Bunge la mwaka 2015 lilikuwa na hiyo live broadcasting, lakini Wabunge wengi hawakurudi. Kitakachowafanya watu wenu wawakubali ni yale mnayotekeleza. Matangazo mubashara hayasaidii chochote, eeh! (Kicheko/Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, halafu kuna hoja imezungumzwa jana hapa, ni aibu! Unasema Serikali hii inaongozwa na watu wasio competent; how can this be? Serikali ni nini? Huyo Rais mwenyewe amekuwemo Bungeni humu tangu mwaka 1995. Mawaziri wanaomsaidia wengi walikuwepo hapa; sisi watumishi wa umma tumekuwemo humu. Mimi nimeanza kazi mwaka 1994. Kinachobadilika ni wanasiasa; nanyi wenyewe mlienda kwenye kura. Mkashindwanishwa walio na uzoefu na wasio na uzoefu. Walio na uzoefu wakashinda, ndiyo wameunda Serikali, mnasema they are not competent. How can this be? This is not seriously at all, we need to be serious! (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, huyo Rais mnayemsema, mimi nilikuwepo pale Ubungo mwezi jana, siku linawekwa jiwe kwenye ujenzi wa barabara sijui mnaita ya magorofa, yule Rais wa Benki ya Dunia alisema hivi; “mimi nimekuja Tanzania kwa sababu huko duniani viongozi wanasema
nenda Tanzania kwanza.” Hatujisifu! Leo udhaifu wa aina gani? Naweza kusema hivyo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninachoweza kushauri Bunge lako Tukufu ni kwamba Serikali hii inaongozwa na watu wanaomudu majukumu yao kwa ufanisi ipasavyo na ndiyo maana imeweza kutekeleza mambo hayo katika muda ambao haujafiakia hata miaka miwili na Serikali imeripoti kupita hizi Wizara mbili na Ofisi ya Waziri Mkuu so far na mwenye macho haambiwi tazama. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ushauri wangu ni kwamba nimemsikia Mheshimwia amesema huu ushirikiano mnaoutaka Serikali ni lazima uanzie humu Bungeni, uta-extend mpaka kwenye majimbo yenu. Hamwezi mkawatukana Mawaziri hapa, Attorney General mnamtukana, Waziri mnamtukana halafu kesho mnasema aje Jimboni kwako, aje kufanya nini?
Mheshimiwa Mwenyekiti, lazima tuwe courtesy. Ni naomba kushauri, Serikali kwa maana ya mihimili yote ya dola, I am talking about the government now.
Executive, Judiciary and Legislation.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho naomba kushauri jambo hili, Serikali kwa maana ya government haiwezi kuruhusu watu wachache wakaharibu mustakabali wa Taifa hili ama kwa vitendo au kwa kauli zao au kwa mienendo zao, ni lazima turudishe nidhamu ndani ya Bunge hili. Ni lazima amani na usalama vitawale.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.