Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Hon. Dr. Harrison George Mwakyembe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyela

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

WAZIRI WA HABARI, UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa fursa hii na nianze kwa kuunga mkono hoja na vilevile kumpongeza sana Mheshimiwa Waziri wa TAMISEMI na mwenzake wa Utumishi na Utawala Bora. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, yamesemwa mengi hapa ambayo yanahitaji ufafanuzi ili tusiupotoshe umma. La kwanza ni kauli tuliyoanza kuisikia jana hapa, imesemwa kwa nguvu hapa, ooh, Mawaziri wa Tanzania ni waoga, hawana ujasiri. Nimekuwa najiuliza, ujasiri wa aina gani? Wa kumkaidi Waziri Mkuu? Kumkaidi Rais? Ujasiri upi wa kukataa pengine three-line whip? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama ni hivyo, umeona wapi dunia ya leo ambapo Mawaziri hawaongozwi na kanuni ya kuwajibika kwa pamoja Bungeni katika Parliamentary system? Hii ndiyo inaitwa collective responsibility, siyo kwamba tumeiokota tu, iko katika Katiba, twende Ibara ya 53.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Ibara ya 53(2) inasema: “Mawaziri, chini ya uongozi wa Waziri Mkuu watawajibika kwa pamoja Bungeni.” Sasa tnapowajibika kwa pamoja Bungeni, aah, hawa sio majasiri.

Nyie mkija kuunda Serikali, maana ni mwaka 2090 huko, bahati nzuri mimi sitakuwepo. Mtakuwa watu gani ambao mna Serikali moja kila mtu anaongea la kwake? Siyo hivyo tu, Waziri Mkuu mwenyewe ambaye sisi tunafanya kazi chini yake, Katiba inasema 53(1), Waziri Mkuu atawajibika kwa Rais kuhusu utekelezaji wake.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hii ndiyo chain ya accountability katika Serikali. Kwa hiyo, tusiwapotoshe wananchi, waoga, tunaogopa kitu gani? Mmeona mtu yeyote anatetemeka hapa? Hatuogopi chochote hapa. (Kicheko)
Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi nashangaa sana, tunapenda kuongelea wenzetu wakati sisi wenyewe tuna...; mimi nimeona, Mheshimiwa Kiongozi wa Upinzani Bungeni alipoingia hapa, watu mpaka mikanda inalegea, wanatetemeka hapa, kimya! Sisi leo kumheshimu Waziri Mkuu wetu ambapo tuna wajibu, lazima tutamheshimu. Lazima! It is our obligation, ni kitu cha ajabu! Tuache mizaha hapa, wananchi wanatuzikiliza, wanatuona we are not serious. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pili, suala la Richmond, hili suala limeibuliwa jana na Mbunge wa Arumeru Mashariki Mheshimiwa Nassari kwamba Kamati Teule iliyochunguza suala hilo haikumtendea haki Mheshimiwa Edward Lowassa kwa sababu haikumhoji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi naelewa, ni kazi ngumu sana leo hii kutaka kumsafisha Mheshimiwa Edward Lowassa kutokana na kesi ya Richmond ambayo ilishakwisha. Ndiyo maana sioni ajabu ili kusema aliyosema, ilibidi Mheshimiwa Nassari anywe pombe kwanza. Ninayasema haya Kiongozi wa Upinzani Bungeni ajue kwamba tuna tatizo hilo. Na mimi ninawapongeza sana vijana wetu wa Usalama waliokamata hiyo chupa hapo. Maana angeruhusiwa na hiyo chupa, huenda hata angetapikia rangi zetu za Taifa humu ndani, ingekuwa ni scandal kubwa kabisa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimeelezea mara nyingi sana katika Bunge hili, hata Bunge la tisa lililoshughulikia suala la Richmond kuwa Kamati Teule iliyoundwa na Bunge hili kazi yake ilikuwa kuchunguza, siyo kutoa maamuzi. Unapochunguza requirement ya audi alteram partem rule, hiyo requirement haipo pale wakati wa uchunguzi; ipo wakati wa maamuzi. Ndiyo maana sisi tulikuja hapa tukaleta kesi hapa tukiwa na mashahidi zaidi ya arobaini wakisubiri nje.
Aliyetakiwa kuhojiwa hapa, akajiuzulu. Unamlaumu Mwakyembe kwa hilo? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba msipotoshe umma. Ooh, hakuhojiwa. Ahojiwe vipi? Unajua ni aibu! Ni sawa na mtu anaenda mahakamani, anasema unajua polisi hawakunipa haki ya kuhojiwa. Polisi? Upo Mahakamani ndipo pakuhojiwa hapo. Pakuhojiwa ilikuwa hapa! Kwa hiyo ndugu zangu, naomba tusipotoshe watu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sisi tulipata nyaraka za Serikali 104; na tukahoji watu 75, tuliwauliza maswali 2,717. Ipo kwenye Hansard! Hatukuona sababu yoyote ya kumwita Mheshimiwa Lowassa. Hatukuona! Tulikuwa na kila kitu, tulikuwa na ushahidi wote. Naomba kama kuna mtu yeyote hapa bado anakereketwa na kesi ya Richmond, aache maneno maneno hapa, alete hiyo kesi iibuliwe kama hatutawanyoa nywele kwa vipande vya chupa, ilete hapa! Acha maneno ya kienyeji hapa! Tumeshachoka! We are tired of this! Jamani eeh, ileteni hiyo kesi hapa, mnaruhusiwa na kanuni.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimalizie kwamba, mimi naahidi, siku ambayo kuna moja atakuwa jasiri hapa kusema nalileta suala la Richmond lirudiwe tena, mimi nitamwomba Mheshimiwa Rais anipumzishe Uwaziri niweze kuishughulikia hii kesi sasa kikamilifu iishe moja kwa moja.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna hoja nyingine aliyoileta hapa kuwa kwenye Ph.D Thesis yangu nilikiri kuhusu Serikali tatu, lakini sasa hivi nasema Serikali mbili.
Anyway, la kwanza ni kwamba kwanza alilewa ndiyo maana alikuwa anasema tu hayo, maana ameambiwa, hajasoma hata hiyo Ph.D Thesis, lakini la pili ni kwamba watu wanaelewa watu wenye integrity, watu wasio na integrity tunawajua hapa ambao wanakesha miaka mitano kumtukana mtu kumwita fisadi, leo wanamkumbatia, wanalamba na nyayo zake, ndio vigeugeu namba moja hao! Halafu leo mnajidai kuja kumsafisha! Huwezi ukasafisha madoa ya lami eti kwa kutumia kamba ya katani au maji, haiwezekani! Lileteni hili suala hapa tulimalize.
Naomba niseme tu kwamba katika ile thesis yangu, naongelea kuhusu mfumo wa two governments, three jurisdictions; na mfumo huo katika hiyo thesis tunasema it is not sui generis; siyo pekee, inatumika katika mataifa mbalimbali yanayotaka ku-partner yakiwa na tofauti kubwa sana ya ukubwa wa eneo, yakiwa na tofauti kubwa sana ya idadi ya watu, yakiwa na tofauti kubwa sana ya rasilimali watu na vilevile maliasili, ndiyo unatumika huo utaratibu. Sasa soma yote, kurukaruka tu, hutaelewa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nilikuwa nasema tu kwamba it is a federal variant, ndiyo hoja kubwa katika hiyo thesis. Kwa hiyo, naomba tu bwana mdogo akipata muda asome kama atapata muda, mimi sijui, mtoto wa Mchungaji yule lakini ndiyo hivyo, ameingia hapa na kachupa ka pombe. (Kicheko)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimalizie suala la mwisho. Naomba nirudie tena, wengine hapa katika kupambana na udhalimu, kupambana na matendo mbalimbali, sisi wengine hapa tumeumia sana, unapoleta masuala hapa kimzaha mzaha; tutakujibu to the maximum. Mimi I am ready for anything. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba akina Mheshimiwa Kubenea na magazeti yao, leteni kesi ya Richmond hapa, nawaomba, chonde chonde, ileteni hapa! Jamani, naomba kwa Mungu, mkiileta hapa, nitafurahi! Kwa sababu ninachosema hapa na ushahidi nilionao hapa ni kwamba sisi tulimkuta huyu jamaa in flagrante delicto, ndivyo wanasema wanasheria, we have everything na mpaka leo hatujafa, tutakuwa hapa kuthibitisha hilo suala.

Kwa sababu mmekuwa na makubaliano ya kumsafisha, hamtaweza kumsafisha. Leteni kesihapa!